Umoja wa Mataifa umesema utaendelea kuwa msitari wa mbele ili kuhakikisha wanawake wanashirikiwa ipasavyo katika masuala ya utafutaji wa amani na usalama na pia ngazi ya maamuzi.
Umoja wa Mataifa pamoja na washirika wake umeanza kuisadia Serikali ya Indonesia kufanya tathmini namna matukio ya tsunami na mlipuko wa volcano ilivyowaathiri wananchi wa eneo hilo.
Mahakama moja inayofadhiliwa na Umoja wa Mataifa kwa ajili ya kuendesha kesi dhidi ya mauwaji ya kiongozi wa zamani wa Lebanon Rafiq Hariri imelaani vikali shambulio kwa watumishi wake kadhaa na ikaonya kwamba vitendo vya namna hivyo havitaitishia mahakama hiyo kuendelea na kazi zake.
Zaidi ya maeneo 15 yanayolindwa yakiwemo ya watawa nchini Mauritania na makao ya nyani afahamikaye kama Orangutangu, Chui na Ndovu yaliyo katika kisiwa cha Sumatra yatapokea dola milioni 6.8 kugharamia jitihada za kulinda maeneo hayo.
Katibu mkuu wa mkataba wa biashara ya kimataifa kwa viumbe vilivyo hatarini Flora na Fauna CITES leo ametangaza kuwa amefanya uamuzi wa kuitunuku serikali ya Thailand kwa juhudi za kulinda viumbe hao.
Mwakilishi maalumu wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia Augustine Mahiga leo amefanya mkutano na Rais wa serikali ya mpito ya Somalia Sheikh Sharif Ahmed na spika wa bunge la nchi hiyo Sharif Hassan Sheikh Aden kwenye uwanja wa ndege wa Moghadishu.
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuratibu masuala ya kibinadamu OCHA limesema taarifa za karibuni za kutimuliwa wakimbizi zaidi ya 150 wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kutoka Angola huenda likazua wimbi jipya la kurejeshwa kwa nguvu wakimbizi katika nchi hizo mbili.
Ripoti mpya ya shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO imetoa wito kwa kilimo cha nchi zinazoendelea kwenda sambasmba na hali ya hewa ili kukabiliana na changamoto za ongezeko la idadi ya watu na mabadiliko ya hali ya hewa.