Kutoka mji wa Oslo, Norway kumeanzishwa rasmi, leo Ijumaa, ushirikiano mpya wa kimataifa wa kuwasaidia mamilioni ya watu wanaogua maradhi ya malaria duniani, hasa wale wanaoishi katika nchi za Asia na mataifa ya Afrika kusini ya Sahara. Mradi huu utawapatia umma huo uwezo wa kumudu dawa za tiba ya malaria, dawa ambazo hunusuru maisha ya mgonjwa, hususan wale watoto wa umri mdogo.