Jumuiya ya Mashirika ya UM Dhidi ya UKIMWI (UNAIDS) imekaribisha uamuzi wa Bunge la Burundi la kukataa ule mswada wa sheria ya kuharamisha usenge na ukhanithi nchini. Michel Sidibé, Mkurugenzi Mkuu wa UNAIDS amewasifu Wabunge kukataa marekibisho hayo, na anaamini kuwa wameonyesha ari kuu ya kutunza haki za binadamu za umma wao, kitendo ambacho anahisi ni cha kupigiwa mfano kwa wabunge wengine wa kimataifa. Kwa mujibu wa taarifa ya UNAIDS, uharamishaji wa tabia ya kijinsiya ya wanaume watu wazima na utenguzi wa haki za binadamu za watu wenye kuishi na virusi vya UKIMWI, ni mambo yenye kukwamisha juhudi za kudhibiti bora maambukizi ya VVU katika dunia, ambazo zinafungamana na fedheha ya uhalifu dhidi ya wasenge.