Katika juhudi za kumarisha uzalishaji na usalama wa chakula walinda amani wa UM kutoka Bangladesh huko Liberia wametenga eka 150 za ardhi kujenga kijiji kipya, kikiwa na shamba la ushirika, ufugaji wa kuku, na kidimbwi cha samaki.
Tume maalum ya idara za UM huko Zimbabwe imesisitiza kwamba hali ya kibinadamu inaendelea kua mbaya sana na kuhimiza serekali na jumuia ya kimatiafa kusaidia kuimarisha juhudi za msaada wa dharura.
Shirika la Afya duniani WHO limesema jumatano kwamba kujitokeza kwa dawa iliyo sugu dhidi ya ugonjwa wa Malaria huko Kusini Mashariki ya Asia inaweza kuhujumu vibaya sana mafanikio ya kimataifa katika kuudhibiti ugonja huo.
Mtaalamu huru wa masuala ya mauwaji ya kiholela UM Philip Alston anasema mauwaji ya kiholela yanayofanywa na polisi wa Kenya ni mambo ya kawaida, yaliyoenea na hupangwa kwa makini.
KM wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon aliwasili Afrika Kusini siku ya Jumanne kuanza ziara yake ya nchi tano za Afrika, itakayomfikisha Tanzania, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Rwanda na Misri.
KM wa umoja wa mataifa Ban Ki-moon aliwasili Afrika Kusini siku ya Jumanne kuanza ziara yake ya nchi tano za Afrika, itakayomfikisha Tanzania, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Rwanda na Misri.
Inaripotiwa kwamba watu 6 wamefariki na wengine 11 hawajapatikana na huwenda wamefariki baada ya wafanyabishara wa magendo kuwalazimisha abiria kuchupa baharini njee ya pwani ya Yemen wiki iliyopita.