Kuanzia mwanzo wa wiki, wajumbe zaidi ya 10,000 wakiwakilisha nchi wanachama karibu 190, pamoja na waangalizi wa mashirika ya kiserekali na yasio ya kiserekali, na vile vile waandishi habari, walikusanyika Kisiwani Bali, Indonesia na kushiriki kwenye mijadala, itakayoendelea kwa majuma mawili, hadi Disemba 14, kuzingatia ajenda ya msingi wa mashauriano kuhusu Mkataba mpya wa kuimarisha udhibiti bora wa mabadiliko ya hali ya hewa duniani katika siku za usoni, hususan baada ya Maafikiano ya Kyoto kukamilisha muda wake katika 2013. Mashaurianio ya kimataifa kuhusu Mkataba mpya baada ya Maafikiano ya Kyoto yanapangwa kukamilishwa 2009.