KM Ban Ki-moon aliwanasihi wajumbe wa kimataifa waliohudhuria Kikao cha Saba juu ua Demokrasia, Maendeleo na Biashara Huru, kilichofanyika Doha, Qatar kuhakikisha duru yao ya mazungumzo itawasilisha mafanikio ya kuridhisha, maana bila ya kuyafannya hayo, alionya, nchi masikini zitaporomoka zaidi kimaendeleo, hali ambayo anaamini itafumsha mitafaruku na kueneza hali ya wasiwasi kwenye mfumo mzima wa biashara katika soko la kimataifa.~