Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Mahojiano

UN News/Assumpta Massoi

Elimu ni mkombozi kwa msichana wa kimasai- Mamasita

Mkutano wa 62 wa Kamisheni ya Hali ya wanawake duniani, CSW62 umeanza makao makuu ya Umoja wa Mataifa, kubwa zaidi linaloangaziwa ni wanawake na wasichana wa vijiji. Wawakilishi wa mashirika ya kiraia wamefika na miongoni mwao ni Maria Mamasita kutoka Monduli mkoa wa Arusha nchini Tanzania.

Sauti
2'8"

Liberia ni mfano kwa nchi zingine zenye migogoro:Opande

Nchi nyingine za Kiafrika zilizo katika vita vya wenyewe kwa wenyewe ziige mfano wa Liberia na kumaliza mizozo ili kunusuru raia wake. Ushauri huo umetolewa na Jenerali mstaafu Daniel Opande aliyekuwa kamanda wa kwanza wa kikosi cha kulinda amani nchini Liberia. Alipozungumza na Zipporah Musau wa idara ya mawasiliano ya umma ya umoja wa Mataifa jenerali msattafu Opande asisitiza hata hivyo haikuwa kazi rahisi kufikia muafaka, kuketi pamoja kujadiliana na kudumisha amani ambayo sasa Liberia inajivunia.

Sauti
3'5"
Sarah Opendi

Bidhaa za tumbaku lazima zidhibitiwe

Bidhaa za tumbaku zinasababisha madhara mengi sana hususani kiafya. Shirika la afya duniani WHO sasa linataka kila nchi mwanachaka kuchukua hatua madhubuti kudhibiti hali hiyo kwa kuweka sheria na kuzitekeleza.

Sauti
2'28"
Jane John (TBC-Tanzania)

Radio haifi ng'o- Jane John

Ujumbe wa siku ya radio duniani mwaka huu wa 2018 ni Radio na Michezo! Umoja wa Mataifa unataka chombo hicho adhimu kitumike kusaidia watu kuchanua na kuonyesha uwezo wao wote. Miongoni mwa watu ambao radio imeweza kuibua stadi zao ni Jane John, mtangazaji wa kike wa habari za michezo katika shirika la utangazaji nchini Tanzania, TBC. Assumpta Massoi alizungumza na Jane kwa njia ya simu kutoka Dar es salaam, Tanzania na kuanza kwa kumuuliza manufaa ya radio!

Sauti
5'10"
UNICEF/Catherine Ntabadde

Mangariba wadondosha nyembe zao Tanzania, wanaume nao wafungua masikio

Nchini Tanzania harakati za shirika la idadi ya watu duniani, UNFPA zimesaidia kuepusha wanawake na watoto wa kike siyo tu dhidi ya mila hatarishi ya ukeketaji au FGM, bali pia zimesaidia kubadili mtazamo wa wanaume kuhusu kuoa wanawake ambao hawajakeketwa. Ali Haji Hamad, afisa wa jinsia kwenye ofisi hiyo amezungumza na Assumpta Massoi kwa idhaa hii.

Sauti
6'15"

Nidhamu ni sababu kuu ya mafanikio- Kiba

Vijana! Umoja wa Mataifa unasema kuwa kundi hili ndilo linalopaswa kuwa mstari wa mbele kutekeleza malengo ya maendeleo endelevu, SDGs. Hii ni kwa kuzingatia siyo tu wingi wao hivi sasa bali pia uwezo wao wa kubuni na kugundua teknolojia bora na fanisi za kufanikisha malengo hayo.

Sauti
4'11"