Ni lazima tutekeleze moja ya madhumuni makubwa ya UN, kulinda raia-FIB
Ulinzi wa amani ni moja ya kazi kubwa ambazo zinatekelezwa na Umoja wa Mataifa kwani migogoro nayo inazidi kushuhudiwa katika nchi mbalimbali.
Ulinzi wa amani ni moja ya kazi kubwa ambazo zinatekelezwa na Umoja wa Mataifa kwani migogoro nayo inazidi kushuhudiwa katika nchi mbalimbali.
Kila mwaka nchini Uganda hutokea wastan wa visa1,850 vya kipindupindu na takriban vifo 45. Hii ni kwa mujibu wa waziri wa Afya wa Uganda Dkt Jane Ruth Acieng alipozungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo.
Visa vingi hutokea sehemu za Mashariki, Kaskazini na Kaskazini Magharibi mwa Uganda. Zoezi hili linadhaminiwa na shirika la kimataifa la muungano wa chanjo ,GAVI na dawa inayotumika ya matone ndio inatumika kwa mara ya kwanza nchini Uganda.
Siraj Kalyango wa Idhaa hii amezungumza na waziri wa afya anehusika na shughuli za jumla , Dkt Sarah Opendi, kuhusu chanjo hii.
Kiswahili kimekuwa na mchango mkubwa kwa wazungumzaji wake hususan Afrika Mashariki kikipigwa jeki na vyombo vya habari kama Radio kwa miaka mingi. Lakini sasa hali ikoje katika kukuza na kuendeleza lugha hii? Ken Walibora ni mwana riwaya na pia amekuwa mwandishi habari akitumia lugha ya Kiswahili miaka nena miaka rudi, Katika mahojiano ,maalum na Siraj Kalyango wa Idhaa hii amezungumzia lugha hiyo na jinsi vyombo vya habari vinavyohusika kuiendeleza.
Tume ya sheria ya kimataifa ya Umoja wa Mataifa mwaka huu wa 2018 imetimiza miaka 70 tangu iasisiwe. Tume hii Imefanya mengi katika kusongesha masuala ya kisheria.
Mkaa, mkaa, mkaa tena mkaa utokanao na miti unatajwa kusababisha uharibifu mkubwa wa mazingira kwa sababu watu wanakata miti na hivyo kuharibu misitu. Misitu ni muhimu siyo tu katika kuweka bayonuai inayohitajika na lishe kwa binadamu, Wanyama na mimea, bali pia hufyonza hewa ya ukaa ambayo inazidi kuongeza ukubwa wa tundu la ozoni kwenye anga kuu.
Kuwa mlemavu sio kulemaa na unastahili kupata haki zote kama wengine , iwe elimu, afya na hata kutoachwa nyuma katika malengo ya maendeleo endelevu au SDG's, amesema seneta wa Kenya ambaye yeye mwenyewe ni mtu mwenye ulemavu.
Mwaka huu Umoja wa Mataifa umeadhimisha miaka 70 ya kuanza kazi rasmi hizo ambazo zimewahusisha wanaume na wanawake ambao wanatumwa sehemu mbalimbali na majukumu tofauti. Katika operesheni hizo 57 zimefanyika tangu mwaka 1988. Pia operesheni nyingi zimetokea barani Afrika.
Walinda amani hao kila mmoja anaiona shughuli hiyo kivyake.Mmoja wa walinda amani wa kikosi hicho anaelezea jinsi kazi ilivyo. Siraj Kalyango wa Idhaa hii amezungumza nae na kuanza kujitambulish ni nani na anafanya kazi wapi.
Umoja wa Mataifa, UN na Muungano wa Afrika, AU wameamua kushirikiana kwa kina ili kusaka suluhu kwenye mizozo na hii imeanza kutekelezwa huko Sudan ambapo ujumbe wa pamoja wa viongozi wa UN na AU uko ziarani nchini humo kutathmini utendaji wa ujumbe wa pamoja wa taasisi hizo huko Darfur, UNAMID.
Matumaini ya maendeleo ya kiuchumi barani Afrika yamepigiwa chepuo na hatua ya hivi karibuni ya kupitishwa kwa azimio la Kigali la Muungano wa Afrika linaloridhia kuanzishwa kwa eneo huru la biashara barani humo.
Matumaini yanaelekezwa Kigali Rwanda ambako nchi za Afrika zinatarajiwa kutia saini makubaliano ya eneo la biashara huru na hivyo kupanua wigo wa soko la bidhaa barani humo.