Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Mahojiano

Dr.Alinda Mashiku

Penye nia pana njia kama nimefika NASA nawe utaweza: Mhandisi Dkt.Alinda Mashiku 

Mwanamke Mtanzania angara kituo cha safari za anga cha Marekani NASA  tawi la Goddard mjini Maryland lililojikita na ufuatiliaji wa safari za satellite. Dkt. Alinda Mashiku ambaye amekuwa NASA kwa miaka minane sasa anasema ilimchukua miaka 12 hadi kuajiriwa NASA kama mhandisi na sasa pia ni meneja wa kitengo cha kuhakikisha satellite zonazokwenda angani hazigongani. Je anahisi vipi kuwa miongoni mwa wanawake wachache wahandisi NASA na safari yake ilianza vipi? Kufahamu yote hayo na mengine mengi ungana na Flora Nducha wa UN News Kiswahili aliyeketi na kuzungumza naye katika makala hii  

Sauti
13'39"

Nidhamu ni sababu kuu ya mafanikio- Kiba

Vijana! Umoja wa Mataifa unasema kuwa kundi hili ndilo linalopaswa kuwa mstari wa mbele kutekeleza malengo ya maendeleo endelevu, SDGs. Hii ni kwa kuzingatia siyo tu wingi wao hivi sasa bali pia uwezo wao wa kubuni na kugundua teknolojia bora na fanisi za kufanikisha malengo hayo.

Sauti
4'11"