Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Mahojiano

UPU

UPU na usongeshaji wa posta kidijitali duniani

Teknolojia ya kidijitali inavyosonga, vivyo hivyo huduma za posta duniani, lengo ni kuhakikisha kuwa posta inakwenda na wakati. Shirika la Umoja wa Mataifa la huduma za posta duniani, UPU linachukua hatua kuona kuwa lenyewe linakuwa kichocheo kwa nchi wanachama kuwa na huduma za posta zinazokwenda na wakati hasa zama za sasa za kidijitali.  Mkurugenzi wa Maendeleo ya Ushirikiano kutoka shirika hilo, Mutua Muthusi anazungumza na Evarist Mapesa wa Idhaa hii na anaanza kwa kuelezea hali ya huduma ya posta hususan katika nchi zinazoendelea au maskini katika zama za sasa za maendeleo ya kidijitali. Mahojiano haya yamefanikishwa na Kayla Redstone wa UPU.

UN News/George Musubao

MONUSCO tuko bega kwa bega na CENI DRC

Tayari Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, Félix Antoine Tshisekedi Tshilombo amethibitisha uchaguzi mkuu utafanyika nchini humo mwishoni mwa mwaka huu kama ilivyopangwa. Sasa ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO  unaeleza ni hatua gani zimefanyika na zinafanyika ili kuhakikisha uchaguzi huo unakuwa huru,a wahaki na unafanyika kwa amani.

Sauti
4'53"
UN News

Dijitali mkombozi kwa mtoto wa kike

Mkutano wa 67 wa kamisheni ya hali ya wanawake duniani CSW67 umekunja jamvi kwenye makao makuu ya UN jijini New York, Marekani na maudhui yalikuwa uvumbuzi, mabadiliko ya kiteknolojia, na elimu katika zama hizi za kidigitali kwa ajili ya kufikia usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa wanawake na wasichana wote. Miongoni mwa walioshiriki ni Elionora Emiel Wilfred, mwanafunzi wa kidato cha 4 katika shule ya sekondari ya Mtakatifu Thereza wa Avila mkoani Kilimanjaro nchini Tanzania. Alizungumza na Selina Jerobon wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa mataifa.

Sauti
5'25"