Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Mahojiano

UN News/Siraj Kalyango

Msikate miti hovyo kwa kuwa jangwa lanyemelea

Ukataji holela wa miti kinyume na vibali ambavyo vinatolewa na serikali ni moja ya sababu za uharibifu wa mazingira nchini Kenya, amesema Isabella Masinde mtaalam wa mazingira, kutoka idara ya mazingira nchini humo.

Katika mahojiano  na Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa  Mataifa mjini New York, Marekani, Bi.Masinde,Mkurugenzi wa Mazingira na ulinzi wa masuala ya  kijamii katika kamati ya kitaifa ya kupokea  malalamiko kuhusu mazingira nchini Kenya amesema.miongoni mwa mengine kuwa maendeleo yanaathiri mazingira   wakati ..mambo ya kufanya mipango ya matumizi ya hayo mazingira hayatekelezwi, lakini kama kungekuwa na utaratibu wa kujua kama kwa mfano miti ikitolewa miti elfu moja tutaendelea vizuri.

Uganda yazindua kampeni ya chanjo dhidi ya kipindupindu-WHO

Kila mwaka nchini Uganda hutokea wastan wa visa1,850 vya kipindupindu na takriban vifo 45. Hii ni kwa mujibu wa waziri wa Afya wa Uganda Dkt Jane Ruth Acieng alipozungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo.

Visa vingi hutokea sehemu za Mashariki, Kaskazini na Kaskazini Magharibi mwa Uganda. Zoezi hili linadhaminiwa na  shirika la kimataifa la muungano wa chanjo ,GAVI na dawa inayotumika ya matone ndio inatumika kwa mara ya kwanza nchini Uganda.

Siraj Kalyango wa Idhaa hii amezungumza na waziri wa afya anehusika na shughuli za jumla , Dkt Sarah Opendi, kuhusu chanjo hii.

Sauti
2'41"

Utamu wa lugha ni pale inapotumiwa kwa ufasaha.

Kiswahili kimekuwa na mchango mkubwa kwa wazungumzaji wake hususan Afrika Mashariki kikipigwa jeki na vyombo vya habari kama Radio kwa miaka mingi. Lakini sasa hali ikoje katika kukuza na kuendeleza lugha hii?  Ken Walibora ni mwana riwaya na pia amekuwa mwandishi habari akitumia lugha ya Kiswahili miaka nena miaka rudi,  Katika mahojiano ,maalum na Siraj Kalyango wa Idhaa hii amezungumzia lugha hiyo na jinsi vyombo vya habari vinavyohusika kuiendeleza.

Sauti
3'19"
UN News/Assumpta Massoi

Methali ya ganda la muwa la jana chungu kaona kivuno sasa ni dhahiri huko Kenya

Mkaa, mkaa, mkaa tena mkaa utokanao na miti unatajwa kusababisha uharibifu mkubwa wa mazingira kwa sababu watu wanakata miti na hivyo kuharibu misitu. Misitu ni muhimu siyo tu katika kuweka bayonuai inayohitajika na lishe kwa binadamu, Wanyama na mimea, bali pia hufyonza hewa ya ukaa ambayo inazidi kuongeza ukubwa wa tundu la ozoni kwenye anga kuu.

Sauti
6'11"
Picha ya UN News/Patrick Newman

Kazi ya Ulinzi wa amani ya UM imefikisha miaka 70.

 

Mwaka huu   Umoja wa Mataifa umeadhimisha miaka 70 ya kuanza kazi rasmi hizo ambazo zimewahusisha wanaume na wanawake ambao wanatumwa sehemu mbalimbali na majukumu tofauti. Katika operesheni hizo 57 zimefanyika   tangu mwaka 1988. Pia operesheni nyingi zimetokea barani Afrika.

Walinda amani hao kila mmoja anaiona shughuli hiyo kivyake.Mmoja wa walinda amani wa kikosi hicho anaelezea jinsi kazi ilivyo. Siraj Kalyango  wa Idhaa hii amezungumza  nae na kuanza kujitambulish ni nani na anafanya kazi wapi.

Sauti
3'33"
UNAMID/Hamid Abdulsalam

Sasa UN na AU zatekeleza ushirikiano kwa vitendo

Umoja wa Mataifa, UN na Muungano wa Afrika, AU wameamua kushirikiana kwa kina ili kusaka suluhu kwenye mizozo na hii imeanza kutekelezwa huko Sudan ambapo ujumbe wa pamoja wa viongozi wa UN na AU uko ziarani nchini humo kutathmini utendaji wa ujumbe wa pamoja wa taasisi hizo huko Darfur, UNAMID.

Sauti
3'13"