Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Dijitali mkombozi kwa mtoto wa kike

Elionora Wilfred akihojiwa na UN News Kiswahili kandoni mwa mkutano wa CSW67 Jijini New York Marekani.
UN News
Elionora Wilfred akihojiwa na UN News Kiswahili kandoni mwa mkutano wa CSW67 Jijini New York Marekani.

Dijitali mkombozi kwa mtoto wa kike

Malengo ya Maendeleo Endelevu

Mkutano wa 67 wa kamisheni ya hali ya wanawake duniani CSW67 umekunja jamvi kwenye makao makuu ya UN jijini New York, Marekani na maudhui yalikuwa uvumbuzi, mabadiliko ya kiteknolojia, na elimu katika zama hizi za kidigitali kwa ajili ya kufikia usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa wanawake na wasichana wote. Miongoni mwa walioshiriki ni Elionora Emiel Wilfred, mwanafunzi wa kidato cha 4 katika shule ya sekondari ya Mtakatifu Thereza wa Avila mkoani Kilimanjaro nchini Tanzania. Alizungumza na Selina Jerobon wa Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa mataifa.