Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Msikate miti hovyo kwa kuwa jangwa lanyemelea

Isabella Masinde,Mkurugenzi wa masuala ya mazingira na ulinzi wa jamii, katika kamati ya kitaifa ya malalamiko kuhusu Mazingira Kenya akihojiwa na UN News katika makao makuu ya UN New York Marekani.

"Mvua inataka ikinyesha maji yake yateremke polepole kwenye miti hadi yafike kwenye nyasi, msipofanya hivyo tutajikuta tuko jangwani.”

UN News/Siraj Kalyango
Isabella Masinde,Mkurugenzi wa masuala ya mazingira na ulinzi wa jamii, katika kamati ya kitaifa ya malalamiko kuhusu Mazingira Kenya akihojiwa na UN News katika makao makuu ya UN New York Marekani.

Msikate miti hovyo kwa kuwa jangwa lanyemelea

Tabianchi na mazingira

Ukataji holela wa miti kinyume na vibali ambavyo vinatolewa na serikali ni moja ya sababu za uharibifu wa mazingira nchini Kenya, amesema Isabella Masinde mtaalam wa mazingira, kutoka idara ya mazingira nchini humo.

Katika mahojiano  na Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa  Mataifa mjini New York, Marekani, Bi.Masinde,Mkurugenzi wa Mazingira na ulinzi wa masuala ya  kijamii katika kamati ya kitaifa ya kupokea  malalamiko kuhusu mazingira nchini Kenya amesema.miongoni mwa mengine kuwa maendeleo yanaathiri mazingira   wakati ..mambo ya kufanya mipango ya matumizi ya hayo mazingira hayatekelezwi, lakini kama kungekuwa na utaratibu wa kujua kama kwa mfano miti ikitolewa miti elfu moja tutaendelea vizuri.