Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ni lazima tutekeleze moja ya madhumuni makubwa ya UN, kulinda raia-FIB

Walinda amani wa Tanzania kwenye kikosi cha kujibu mashambulizi, (FIB) cha ujumbe wa Umoja wa Mataifa huko DRC, MONUSCO. (Picha:MONUSCO/Force)

Ni lazima tutekeleze moja ya madhumuni makubwa ya UN, kulinda raia-FIB

Amani na Usalama

Ulinzi wa amani ni moja ya kazi kubwa ambazo zinatekelezwa na Umoja wa Mataifa kwani migogoro nayo inazidi kushuhudiwa katika nchi mbalimbali.

Kazi hii muhimu inayotekelezwa na Umoja wa Mataifa inahitaji ushirikiano na nchi wanachama kwani wao ndio wanachangia vikosi vya kulinda amani katika nchi wanakohitajika. Licha ya umuhimu wa wajibu huo lakini hapakosi changamoto zinazokabili nchi zinazochangia katika kufanikisha ulinzi wa amani. Moja ya nchi ambazo zinachangia walinda amani ni Tanzania ambapo hivi karibuni wamefanya mkutano wa pande mbili na Umoja huo kujadili mabadiliko na changamoto katika operesheni za ulinzi wa amani.

Meja Jenerali Alfred Fabian Kapinga ni mkuu wa operesheni na mafunzo wa jeshi la wananchi wa Tanzania (JWTZ), amezungumza na Flora Nducha wa Idhaa hii akiangazia ikiwemo mkutano wao na UM, hapa anaanza kwa kuelezea mkutano ulihusu nini? 

Soundcloud