Mkutano wa Umoja wa Mataifa Wakuu wanchi wa Kubadilisha Elimu, Kujenga Mustakabali Wetu wa Baadae utafanyika katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani mwezi Septemba 2022 ili kushughulikia matatizo madogo na yasiyoonekana ambayo watoto na vijana duniani kote wanakabiliana nayo, ambayo ni usawa, ushirikishwaji, ubora na umuhimu.
Mkutano huo unatarajiwa kutoa fursa ya kuinua elimu katika ajenda ya kisiasa ya kimataifa na kuhamasisha hatua kuchukuliwa ili kurejesha hasara zilizoikumba sekta ya elimu zilizosababishwa na janga la COVID-19 na kupanda mbegu ili kubadilisha ambayo itasaidia kuleta mabadiliko makubwa ya kasi katika elimu ulimwenguni kote.
Haya ni baadhi ya madhila yanayowasibu watoto kutoka katika kila pembe ya dunia.
Wakati shule nyingi zikiwa zimekaliwa na wanajeshi au kutoweza kufikiwa kwa urahisi kutokana na migogoro, kuhama na kukosekana kwa utulivu, Jamhuri ya Afrika ya Kati (CAR) imekuwa mojawapo ya maeneo magumu zaidi duniani kuwa mtoto.
Kwa sababu watoto wanahitaji kupata nafasi salama za kujifunzia na elimu bora, Shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia watoto duniani UNICEF linatanguliza maamuzi yanayozingaia kuwanufaisha watoto na kuwahakikishia usalama wao na wanafunzi kurejea shuleni kwa usalama huku pia wakitengeneza miundombinu endelevu ya maji, usafi wa mazingira na usafi katika maeneo ambayo hayajahudumiwa.
Huku kukiwa na mzozo na ukosefu wa usalama unaoendelea nchini Niger na eneo jirani la Sahel, pamoja na kufungwa kwa shule kulikosababishwa na janga la COVID-19, wanafunzi wengi wameshindwa kuhudhuria madarasa hali inayowaweka matatani kufanyiwa unyonyaji na unyanyasaji.
UNICEF inatetea uingiliaji kati ili watoto wote waweze kupata elimu bora, kama vile kuboresha ufikiaji wa elimu bora, huduma za mabadiliko ya tabia na kijamii, utoaji wa mgao bora wa bajeti ya elimu kutoka serikalini.
Kati ya wimbi la wakimbizi na mzozo wa kiuchumi ambao umezidishwa na janga la COVID-19, shule za nchini Lebanon zimepata pigo kubwa, hata kama Jimbo lililodorora linakabiliwa na mahitaji ya kuongezeka ya elimu inayofadhiliwa na umma na kuongezeka kwa idadi ya wanafunzi walioacha shule, watoto wenye rasilimali chache tu.
Kwa ushirikiano wa karibu na Sekta ya Elimu, yakiwemo mashirika ya Umoja wa Mataifa, Wizara ya Elimu imeandaa mkakati wa miaka mitano wa kukabiliana na elimu unaolenga kuboresha upatikanaji wa elimu na ubora wa huduma na mifumo ya elimu.
Hata kabla ya misaada mingi ya kimataifa kukatizwa nchini Afghanistan baada ya Taliban kushika madaraka mwaka jana, miongo kadhaa ya migogoro, umaskini na ukame wa muda mrefu vimesababisha nusu ya watu wakihangaika kuweka chakula mezani na karibu wasichana na wavulana milioni 10 wakitegemea msaada wa kibinadamu kuishi.
Kati ya watoto wanaokadiriwa kufikia milioni 3.7 ambao hawako shuleni nchini humo, asilimia 60 kati yao ni wasichana, kulingana na UNICEF, ambayo inatetea elimu yao kama hitaji la kimaadili na la kiuchumi.
Baada ya miaka saba ya mzozo nchini Syria, migogoro, kufurushwa, na ukosefu wa usalama pamoja na ukosefu wa nafasi za kujifunzia na walimu waliohitimu kumesababisha mamilioni ya watoto kukosa elimu.
Pamoja na zaidi ya shule 7,000 kuharibika au kubomolewa, kugeuka kuwa vituo vya kusaidia watu, madarasa yaliyotengenezwa awali yanalengwa kuwarejesha wanafunzi katika masomo yao pamoja na mafunzo ya ualimu, programu mbadala za kujifunza na nyenzo muhimu za kufundishia zinazokidhi mahitaji ya watoto shuleni na katika jamii.
Kwa mujibu wa takwimu za kitaifa, watoto 11,842 wenye ulemavu nchini Cuba idadi ambayo ni takriban nusu yao wanatatizika kiakili, wanasoma shule za kawaida, kama sehemu ya mchakato wa elimu mjumuisho.
Ndani ya mfumo wa elimu ya jumla, elimu mjumuisho hutoa elimu muhimu kwa wanafunzi wote, kuruhusu wanafunzi walio na ulemavu na wasio na ulemavu kuhudhuria madarasa yanayolingana na umri, kwa usaidizi wa kibinafsi kama inahitajika.