Mradi unaofadhiliwa na Umoja wa Mataifa unawasaidia Wananachi wa wilaya ya Korolevu-i-wai nchini Fiji kuendesha miradi ya utalii endelevu inayohusishwa na miamba ya matumbawe na kusaidia mahitaji ya maendeleo ya jumuiya.
Victor Bonito, mwanaikolojia wa miamba ya matumbawe, amekuwa akifanya kazi na jumuiya ya wenyeji tangu mwaka 2005, ili kuwasaidia kusimamia vyema na kurejesha rasilimali za baharini katik uvuvi wa asili.
Akifanya kazi katika utafiti wa miamba ya matumbawe na juhudi za uhifadhi duniani kote kwa zaidi ya miaka 22, Victor ana ujuzi wa kina wa mifumo ya ikolojia ya miamba ya matumbawe.
Ustadi huu ni muhimu sana katika nchi kama Fiji, ambako kisiwa chenye watu wengi zaidi - Viti Levu – kilicho pembezoni mwa pwani yake ya kusini-magharibi na mfumo wa miamba mirefu zaidi nchini humo, unaojulikana kama Pwani ya Matumbawe.
Mpango wa Uwekezaji katika Miamba ya Matumbawe na Uchumi wa Bluu (ICRBE) unasaidia wamiliki wa haki za kimila za uvuvi kwa jumuiya ya Korolevu-i-Wai, kuendesha kwa uendelevu vivutio na shughuli za utalii wa kimazingira zinazohusiana na miamba ya matumbawe katika Eneo la Bahari linalosimamiwa ndani ya maeneo husika, pamoja na kusaidia mahitaji ya maendeleo ya jamii ya jamii.