Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa Maendeleo Duniani UNDP nchini Pakistani, linafadhili mradi unajumuisha takriban hekta 145,300 lengo likiwa ni kulinda miti iliyohatarini kupotea na aina muhimu za miti ya msituni huko Punjab, pamoja na misitu iliyo karibu na kingo za mito huko Sindh.
Inakadiriwa kuwa chini ya asilimia 5 ya eneo lote la ardhi ya Pakistani limezingirwa na misitu na karibu asilimia 1.5 ya misitu ya Pakistani hupotea kila mwaka.
Maeneo haya yaliyo hatarini pia yanatoa ishara ya hatari kwa sababu yana rutuba bora na nzuri ambayo huwavutia wakulima ambao wanataka kupanua eneo lao. Mradi ulizindua shughuli ya kuchora ramani na kuweka mipaka ya ardhi hizi za misitu, ili kuhifadhi misitu yenyewe, na pia kuhifadhi huduma zao za mfumo ikolojia.
Wakati misitu inakatwa kwa kuchagua maeneo maalum, inaweza kurejeshwa kwa juhudi za kawaida na mbinu rahisi ambazo huruhusu kuhifadhi bioanuwai na kupunguza mabadiliko ya tabianchi. Kinyume chake, ikiwa ukataji ni mkubwa zaidi, upandaji miti unahitaji juhudi kubwa katika viwango vyote vya kijamii, kisiasa na kisheria.
Jumla ya hekta 83,350 za ardhi ya misitu zilipimwa, na hekta 2,024 za ardhi ya misitu zilirudishwa kutoka kwa wavamizi katika maeneo ya ardhi mawili ndani ya mradi huo unaofadhiliwa na UNDP.
Thamani ya chini inayokadiriwa ya ardhi iliyorudishwa katika jimbo la Sindh pekee ni dola milioni 10.