Jumuiya ya kimataifa imekaribishwa tena kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, kwa ajili ya mjadala wa kila mwaka wa viongozi wa dunia ambao mwaka huu unafanyika ana kwa ana na pia mtandaoni, baada yam waka jana kuvurugwa na janga la corona au COVID-19.
Brazil kama kawaida huwa ni mjumbe wa kwanza kutoa kutoka nchi wanachama kuhutubia mjada mkuu wa Baraza Kuu na mwaka huu Rais Jair Bolsonaro alifika kutoa hotuba yake ana kwa ana
BTS wamekuja kuchagiza tukio lililoshajihishwa na mtangazazi wa kituo cha Habari cha ABC, Juju Chang, lililojikita na SDGs au malengo ya maendeleo endelevu ambayo yako 17 yakilenga kupunguza umasikini , kulinda sayari dunia na kujenga dunia iliyo na usawa zaidi.
Na katika eneo la uwanja wa Umoja wa Mataifa North Lawn nje kidogo ya ukumbi wa Baraza Kuu msanii wa Uswiss Saype amewasilisha kazi yake ya sanaa "World in Progress II", au dunia iko katika mchakato sehemu ya pili ambayo inaonyesha Watoto wawili wakifanya takwimu za origami zinazowakilisha dunia ya baadaye wanayoitaka.
Mjadala wa ngazi ya juu wa mwaka huu wa UNGA76 unatarajiwa kufanyika kwa wiki moja.