Miaka kumi baada ya tetemeko la ardhi nchini Haiti ambalo liliwaua watu takriban 220,000, ukumbusho ulifanywa katika Umoja wa Mataifa kuwaenzi wafanyikazi 102 wa Umoja wa Mataifa waliofariki dunia katika tukio hilo. Gregory Grene anagusa jina la kaka yake, Andrew, ambaye alikuwa mmoja wa waathirika.
Miaka sabini na tano baada ya ukombozi wa kambi ya mateso ya Ujerumani ya Nazi ya Auschwitz, ambapo karibu Wayahudi milioni waliuawa, manusura walikusanyika katika Umoja wa Mataifa kuashiria Siku ya ukumbusho ya Holocaust au mauaji ya maangamizi makubwa. Mmoja wao, Sal Birenbaum, anaonyesha nambari iliyochorwa kwenye mkono wake.
Waandishi wa habari kutoka ulimwenguni kote huripoti kutoka ndani ya jengo la Umoja wa Mataifa. Mikutano ya waandishi wa habari ya hadharani, inayojulikana kama stake-outs, hufanyika nje ya chumba cha Baraza la Usalama. Hapa, Katibu Mkuu António Guterres akielezea waandishi wa habari kuhusu hali ilivyo nchini Libya
Mnamo Januari 19, Katibu Mkuu wa awali na wa tano wa Umoja wa Mataifa, Javier Perez de Cuéllar, alisherehekea siku yake ya kuzaliwa ya 100. Picha yake iko pamoja na zile za Makatibu Wakuu wengine saba wa zamani kwenye ukumbi wa jengo la makao makuu ya Umoja wa Mataifa.