Mwanamke huyu mwenye umri wa miaka 30, ambaye ana watoto watano alikimbia kijiji chake miaka miwili iliyopita wakati wanaume wenye silaha walivuka kutoka Nigeria usiku wa manane na kuchoma nyumba yake kijijini Maroa. Akizungumza na UN News amesema kwamba hajamwona mumewe tangu hapo na kwamba baada ya shambulio hilo la Boko Haram maisha yake yaliangamia na kwamba kuuza bidhaa hizi kunamsaidia kujenga tena maisha yake.
Boko Haram na vikundi vingine vya waislamu wenye misimamo mikali wameendeleza mashambulizi ya kigaidi Kaskazini-mashariki mwa Nigeria na Cameroon. Umoja wa Mataifa uliunga mkono uhamiaji wa hivi karibuni wa zaidi ya raia 35,000 wa Nigeria kuingia Cameroon baada ya mji wa Rann nchini Nigeria kushambuliwa na watu hao wenye misimamo mikali.