Nchini Venezuela, mzozo unaoendelea wa kiuchumi na kisiasa umesababisha zaidi ya watu milioni 4, sawa na zaidi ya asilimia 10 ya wananchi wa taifa hilo la Amerika ya Kusini, wakimbie nchi hiyo na kusaka hifadhi nchi jirani za Colombia, Brazil na sasa Peru.
Kamishna Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR Filippo Grandi (pichani) akiwa na familia iliyorejea Damascus, Syria kufuatia kupungua kwa ghasia. Akizungumzia siku ya wakimbizi duniani, Bwana Grandi amesema kuelekea siku ya wakimbizi duniani tarehe 20 Juni, "tumeshindwa kuweka mazingira ya amani."
Nchini Yemen, asilimia 80 ya wananchi wamenasa kwenye mtego ambao mkuu wa ofisi ya usaidizi wa kibinadamu ya Umoja wa Mataifa, amefafanisha na mtego wa panyabuku ambao kila akijaribu kujinasua anashindwa. Ni mtego uliozingirwa na magonjwa, viwa na machungu. Iadi kubwa ya wananchi hawana makazi na wanaishi katika mazingira ambamo kwayo wanapata mahitaji hata yale ya msingi wanakosa.
Hivi sasa kuna takribani wakimbizi 910,00 wa kabila la Rohingya waliosaka hifadhi nchini Bangldesh. Wengi wao waliwasili nusu ya pili ya mwaka jana na baadhi yao kama Narun Nahar(pichani) wanaweza kujipatia kipato kidogo kwa kutoa huduma kama vile kushonea nguo wakimbizi wengine.