Sweden ilianza kuchangia vikosi kwenye operesheni za ulinzi wa amani za Umoja wa Mataifa mwaka 1948 na tangu wakati huo zaidi ya wanawake na wanaume 80,000 kutoka Sweeden wameshiriki operesheni mbalimbali za ulinzi wa mani za Umoja wa Mataifa ikiwemo kwenye kikosi cha dharura cha Umoja wa Mataifa nchini Misri (UNEF) mwaka 1956 kama wanavyoonekana pichani. UN Photo/GJ
Wanawake siku zote wamekuwa na mchango na jukumu muhimu katika operesheni za ulinzi wa amani za Umoja wa Mataifa. Wanawake 12 kutoka kikosi cha askari watembea kwa miguu walikuwa wanawake wa kwanza walinda amani kujiunga na mpango wa Umoja wa Mataifa nchini Cyprus, UNFICYP, 1979. UN Photo/John Isaac
Nchini Sudan Kusini, Sweden imepeleka maafisa wa polisi ambao ni sehemu ya mpango wa Umoja wa Mataifa nchini humo UNMISS. Hawa ni baadhi ya maafisa hao wa polisi wa wakichangamana na wakimbizi wa ndani katika moja ya makazi ya ulinzi wa Rais ya Umoja wa Mataifa mjini Juba.UNMISS/Nektarios Markogiannis
Nchini Timor Leste, mwaka 2010, maafisa wa polisi kutoka Sweden wakiwa sehemu ya mpango wa Umoja wa Mataifa nchini humo, UNMIT. Hapa afisa kutoka Sweden akiwa pamoja na mwenzake wa kutoka China wakiwa kwenye kituo cha kulea watoto yatima kwenye mji mkuu Dili.