Waandishi wa hati mkato walitegemewa sana wakati huo. Hata hivyo binadamu ni binadamu, anaweza akakosa neno moja na hivyo kuharibu mwenendo mzima. Ili kuepusha hali hiyo, mashine kama hiyo pichani ilitumika kunasa sauti ili kuhakikisha kilichoandikwa ni sawa na kilichorekodiwa na mashine .
Wajumbe huwa wana saa 48 kuhakiki hotuba zao na pia kuweza kutuma masahihisho kwa wahariri ili yaweze kuyajumuishwa katika nakala iliofanyiwa marekebisho. Kazi hiyo ni ngumu kama vile kukagua herufi na maandishi kuwa ni sawa na huweza kuandikwa kwenye ubao ili kuona kwamba kuna uwiano.
Nyaraka tayari zimekamilika, na pichani ni nyaraka rasmi za Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa. Iliyofunguliwa iko katika lugha ya kirusi, ilihali nyaraka zingine ni katika lugha nyingine rasmi za Umoja wa Mataifa ambazo ni Kiingereza, Kifaransa, Kichina na Kispanyola.