Zaidi ya miaka 50 ya anga kwa mustakabali bora wa dunia


Disemba 1958: Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa lapitisha azimio kuhusu “Hoja ya matumizi ya amani ya anga la juu” na kutambua maslahi ya pamoja ya kibinadamu ya anga hilo kwa faida ya wote. Mwaka uliofuatia Kamati ya matumizi ya amani ya anga za juu ilikutana kwa mara ya kwanza (pichani) katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa New York.

Oktoba 1963: Mwanaume na mwanamke wa kwanza kwenda anga za juu. Yuri Gagarin (kulia) na Valentina Tereshkova ( wa pili kushoto) watembelea makao makuu ya Umoja wa Mataifa. Pichani wanaonekana na Katibu Mkuu U Thant (wa pili kulia) na Rais wa Baraza Kuu Carlos Sosa-Rodriguez (kushoto).

Disemba 1963: Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa linapitisha “Azimio la Kanuni za kisheria zinazoongoza shughuli za Mataifa katika Uchunguzi na Matumizi ya anga za juu, " na kuanzisha sheria ya anga za juu kama chombo kipya cha sheria.

Julai 1969: Bendera ya Umoja wa Mataifa inaambatana na wanaanga wa Marekani Neil Armstrong, Edwin Aldrin Jr na Michael Collins kwenye safari ya mwezini ya Apollo 11. Pichani ni wataalamu watatu, Armstrong , (wa pili kushoto), Aldrin, (wa tatu kulia) na Collins, (wa pili kulia) wanatembelea makao makuu ya Umoja wa Mataifa, na Katibu Mkuu U Thant (katikati) akiwa na jiwe kutoka mwezini na bendera (Julai 1970) .

Novemba 1995: Wanaanga wa chombo cha pili cha anga za juu cha Mir Docking wakiwa wameshikilia nakala ya mkataba wa shughuli za anga za juu, ambao walitia saini wakiwa anga za juu katika kusherehekea maadhimisho ya miaka 50 ya Umoja wa Mataifa.

Novemba 1995: Katibu Mkuu Boutros Boutros-Ghali akizungumzia kupitia video na wanaanga wakati wa maadhimisho ya miaka 50 ya Umoja wa Mataifa

Mei 2004: Yang Liwei, mwanaanga wa kwanza wa kichina kusafiri anga za juu anakukutana na Katibu Mkuu Kofi Annan. Wakati wa mkutano huo, Bw. Liwei alimpatia mkuu huyo wa Umoja wa Mataifa bendera ya Umoja wa Mataifa iliyopeperushwa kwenye chombo cha anga za juu cha Shenzhou 5.

Juni 2011: UN inaadhimisha miaka 50 ya shughuli za anga kwa mwanadamu kwa maonyesho yaliyofanyika kwenye chumba cha mkutano cha kituo cha kimataifa ha Vienna.

Juni 2013: UN inaadhimisha miaka 50 ya wanawake katika anga za juu kwa kujumuisha viongozi wanawake kwenye sekta hizo wakati wa kikao cha kamati ya matumizi ya anga za juu kwa amani huko mjini Vienna, Austria.

Novemba 2016: Umoja wa Mataifa wamteua mwana anga wa zamani wa Marekani, Scott Kelly, ambaye alikaa kituo cha kimataifa cha anga za juu kwa muda wa mwaka mmoja kuwa bingwa wa kuhamasisha manufaa ya anga za juu kwa maendeleo endelevu. Pichani Bw. Kelly (kushoto) na Simonetta Di Pippo (kulia), Mkurugenzi wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa masuala ya anga za juu (UNOOSA).