Jumla ya operesheni 71 za ulinzi wa amani za Umoja wa Mataifa zimeshatumwa katika nchi mbalimbali na 57 kati ya hizo tangu mwaka 1988.
Vikosi vya ulinzi wa amani wa Umoja wa Mataifa vilianzishwa wakati wa vita vya baridi vya dunia ambapo mahasimu katika vita hivyo walitumia nafasi zao kupinga maazimio ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa .
Hapo awali ulinzi wa amani ulikuwa na jukumu moja tu la kusimamia makubaliano ya amani kama ilivyo pichani kwenye eneo la Jammu na Kashimir ambako kundi la uangalizi wa kijeshi la UN limekuwepo tangu mwaka 1949 kusimamia sitisho la mapigano kati ya India na Pakistani.
Walinda amani wa kwanza kubeba silaha walitumwa mwaka 1956 kwenye operesheni ya dharura ya kusimamia mtafaruku wa Suez.
Jukumu lao lilikuwa kusaidia kumaliza uhasama, ikiwemo kuondoka kwa majeshi ya Ufarasan, Israel na Uingereza kutoka eneo la Misri na pia kusaidia kama ukuta kati ya majeshi ya Misri na Israel. Walinda amani walitumia njia zozote za usafiri walizokuwa nazo ili kufanya kazi yao.
Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini DR Congo -ONUC mwaka 1960 inasadikiwa kuwa operesheni kubwa ya walinda amani 20,000 kwa wakati mmoja .
Katika operesheni hiyo walinda amani 250 walipoteza maisha ikimjumuisha Katibu Mkuu wa UmMoja wa Mataifa General Dag Hammarskjold aliyefariki dunia kwa ajali ya ndege wakati akielekea eneo hilo kusaka makubaliano ya amani. (Pichani) Walinda amani kutoka India wakimsaidia mwenzao majeruhi. Na hadi leo hii walinda amani wa UN bado wako DR Congo.
Mwishoni mwa vita baridi vya dunia, mikakati ya ulinzi wa amani kwa vikosi vya walinda amani ulibadilika kutoka kusimamia tu makubaliano ya amani hadi ufuatliaji na utekelezaji wa mikataba ya amani.
(Pichani) Walinda amani kutoka Uholanzi wakiwa Cambodia mwaka 1991 kusimamia mchakato wa amani baada ya uchaguzi, na pia kusaidia katika masuala ya haki za binadamu, utawala wa sheria na pia ujenzi wa miundombinu
Kumekuwepo na operesheni nyingi zaidi za ulinzi wa amani Afrika kuliko popote duniani.
Operesheni hizo katika nchi za Afrika madharibi kama Liberia, Sierra Leone na Ivory Coast zilimalizika kwa mafanikio makubwa baada ya migogoro iliyodumu kwa muda mrefu. (Pichani) Mlinda amani wa Umoja wa Mataifa nchini Liberia akiwa katika operesheni ya kutokomeza matumizi ya silaha.
Miaka ya hivi karibuni idadi kubwa ya wanawake wamekuwa wakitumwa katika operesheni mbalimbali za ulinzi wa amani katika Umoja wa Mataifa .
Katika operesheni ya ulinzi wa amani nchini Mali, kuna wanawake 38 kutoka Burkina Faso ambao wanasaidia katika shughuli ulinzi wa raia walioko katika makambi yanayosimamiwa na Umoja wa Mataifa.
Nchini Sudan Kusini, miaka miwili baada ya uhuru wa nchi hiyo mwaka 2011, vita vya wenyewe kwa wenyewe viliibuka.
Askari wahandisi wa Umoja wa Mataifa walikarabati barabara kadhaa. Ufikishaji wa misaada ya kibinadamu umeimarika, halikadhalika doria zinazofanywa na walinda amani ikimaanisha wakazi wanajisikia wako salama. Pichani ni barabara karibu na Pirbo, mashariki mwa nchi abmayo ilikarabatiwa na wahandisi wa Korea Kusini na sasa imechochea biashara na kuongeza upatikanaji wa bidhaa sokoni.
Miaka 70 tangu operesheni ya kwanza ya ulinzi wa amani ya Umoja wa Mataifa, bado kuna operesheni 14 za ulinzi wa amani kote duniani
Operesheni za ulinzi wa amani zimebaki kuwa kazi ngumu na hatari kuwahi kutokea duniani. Zaidi ya walinda amani 3700 wamepoteza maisha yao katika operesheni hizo tangu mwaka 1948.
Mashambulizi dhidi ya walinda amani wa Umoja wa Mataifa yamesababisha Mali kuwa nchi hatari zaidi kutokana na mashambulizi ya mara kwa mara dhidi ya walinda amani. Pichani ni mazishi wa walinda amani kutoka Chad na Nigeria waliouwawa katika mashambulizi ya mwezi Aprili mwaka huu.