Kwa miongo sasa Indonesia imetoa mchango muhimu katika ulinzi wa Amani wa Umoja wa Mataifa, wakihudumu katika baadhi ya maeneo yenye changamoto kubwa ikiwemo jimbo la darfur Sudan, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC na Sudan kusini. Wanaonekana hapa wakiwa katika wasaa wa kuagana kwa mfumo wa tamaduni za Indonesia, ni kikosi cha Garuda cha jeshi la serikali ya Indonesia wakati kikosi hicho kikijiandaa kuondoka Jarkata mwezi Septemba 1960 kwenda kuhudumu kwenye jeshi la umoja wa Mataifa Congo. Kulia ni Kapteni Andjar Rachman, Kamanda msaidizi wa kikosi hicho.
Picha na UN/KAR
Miongoni mwa maelfu ya wanawake na wanaume wa Indonesia waliohudumua katika operesheni za ulinzi wa Amani za Umoja wa Mataifa ni Rais wa zamani wan chi hiyo, Susilo Bambang Yudhoyono, ambaye mbali ya kuwa mlinzi wa Amani wa Umoja wa Mataifa , bwana Yudhoyono (kulia) na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa wakati huo Ban Ki-moon (wa pili kulia) wakiwa wamevalia Bereti za bluu huku wakiangalia vifaa vya ulinzi wa Amani kwenye kituo cha Amani na usalama cha Indonesia mjini Jarkata wakati wa ziara ya Katibu Mkuu mwezi Machi 2012.
Picha na UN/Eskinder Debebe
Wajumbe wa kikosi cha Indonesia kwenye mpango wa Umoja wa Mataifa wa kulinda Amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR ujulikanao kama (MINUSCA), Ikiwa ni mwezi Agosti 2014, miongoni mwa vikosi vya kwanza kuwasili baada ya Baraza la Usalama kupiga kura ya kupeleka vikosi vya kulinda Amani kusaidia kurejesha utulivu nchini humo baada kuzuka machafuko mabaya baina ya jamii tofauti.
Picha na UN/Catianne Tijerina
Walinda amani wa Umoja wa Mataifa wakati wa uzinduzi wa mradi wa ujenzi wa barabara mjini Bangui , mji mkuu wa CAR mwezi Septemba mwaka 2014. Mradi huo wa ujenzi uliendeshwa na walinda Amani wa Indonesia kwa ushirikiano na wahandisi wa wizara ya ujenzi ya nchi hiyo.
Picha na UN/Catianne Tijerina
Wanaoonekana hapa ni wafanyakazi wa kampuni ya uhandisi ya Indonesia wanaohudumu kwenye mpango wa Umoja wa Mataifa wa kudumisha Amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo(MONUSCO) wakikarabati daraja la Gada , lililopo kilometa 74 kutoka mji wa Dungu, daraja hili limekuwa na jukumu muhimu sana katika kusaidia wenyeji wa eneo hilo na kuimarisha uwezo wa MONUSCO kufika maeneo mbalimbali. (16 Mai 2016)
Picha na MONUSCO/CPL Hasanuddin
Luteni Kanali Yenni Windarti, mjumbe wa kikosi cha polisi cha Indonesia kwenye mpango wa UNAMID akizungumza na wanawake na watoto eneo la kuteka maji kwenye kambi ya wakimbizi wa ndani ya Abu Shouk wakati wa diria ya asubuhi mjini El Fasher, Kaskazini mwa Darfur. Mwezi Agosti 2012, Indonesiailikuwa na polisi 150 kwenye kikosi cha Umoja wa Mataifa jimboni Darfur Sudan ili kuwasindikiza na kutoa ulinzi kwa wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa na wakazi wa kambi za Abu Shouk na Zam Zam
Picha na UN/Albert González Farran
Mwezi Agosti 2015, kikosi cha Indonesia kilikabidhi pampu ya mkono ya maji kwenye kambi ya wakimbizi wa ndani ya Al Riyad, Magharibi mwa Darfur. Miradi kama hiyo mara nyingi huendeshwa na walinda amani wa UNAMID kwa mkakati wao wenyewe wa kuwasaidia wahitaji na kuboreshmaisha ya kila siku ya jamii za eneo hilo.
UN Photo/Muntasir Sharafdin
Kuanzia tarehe 31 Machi 2018, Indonesia imekuwa mchangiaji wa 8 mkubwa wa vikosi na polisi kwenye operesheni za ulinzi wa Amani za umoja wa Mataifa ikiwa na jumla ya wahudumu 2, 700 kwenye operesheni hizo. Pichani ni walinda Amani wa UNAMID kutoka Indonesia wakiendesha kampeni ya tiba kwenye kambi ya wakimbizi wa ndani ya Zam Zam Kaskazini mwa Darfur Februari 2017, wakitoa huduma ya bure ya uchunguzi wa afya kama sehemu ya huduma zao kwa jamii.
Picha na UN/Amin Ismail
Walinda amani wa Indonesia wanaohudumu kwenye kikosi cha Umoja wa Mataifa nchini Lebanon (UNIFIL) wakiwa katika doria maeneo ya vijijini karibu na Taybe, Kusini mwa Lebanon, mwezi Julai 2009. Ikiwa na wahudumu zaidi ya 1,200 Indonesia ndio mchangiaji mkubwa wa vikosi kwa UNIFILuniformed tangu ,Februari 2018.
Picha na UN/Pasqual Gorriz
Historia ya kujivunia ya Indonesia katika huduma za operesheni za ulinzi wa amani za Umoja wa Mataifa haijaja bila kulipa gharama kubwa kwani raia wake 36 wamepoteza Maisha wakati wakihudumu kwenye operesheni za Umoja wa Mataifa. Pichani ni walinda Amani wa Indonesia na Ufaransa wakiwa katika doria ya pamoja karibu na mji wa Taybe, Kusini mwa Lebanon, mwezi Julai 2013.
Picha na UN/Pasqual Gorriz