Kikao cha Kamisheni ya Hali ya wanawake mwaka huu CSW 70 kinafanyika kuanzia tarehe 09 -19 Machi 2026.
Maudhui ya kipaumbele kwa mwaka 2026 ni kuhakikisha na kuimarisha upatikanaji wa haki kwa wanawake na wasichana wote, ikiwa ni pamoja na kwa kukuza mifumo ya sheria iliyo jumuishi na yenye usawa, kuondoa sheria, sera na vitendo vya kibaguzi, pamoja na kushughulikia vikwazo vya kimuundo vinavyozuia upatikanaji wa haki.
Washiriki wakionesha furaha baada ya kupitishwa kwa rasimu ya azimio lenye kichwa cha habari "Tamko la Kisiasa wakati wa maadhimisho ya miaka thelathini ya Mkutano wa Nne wa Dunia kuhusu Wanawake" wakati wa ufunguzi wa kikao cha sitini na tisa cha Kamisheni ya Hali ya Wanawake mwezi Machi 2025. Azimio hilo, lililopitishwa kwa makubaliano, linathibitisha tena ahadi za Azimio la Beijing na Jukwaa la Utekelezaji, lililopitishwa awali mwaka wa 1995 katika Mkutano wa Nne wa Dunia kuhusu Wanawake, likisisitiza hitaji la kutetea haki zote za binadamu na uhuru wa msingi kwa kila mwanamke na msichana, bila ubaguzi.
CSW inakuza haki za wanawake na wasichana, inaandika na kuweka kumbukumbu ya hali halisi ya maisha yao katika sehemu mbalimbali duniani, na pia inaweka mwelekeo wa viwango na sera za kimataifa kuhusu usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa wanawake na wasichana.