Nikuze, mwenye umri wa miaka 12, ameandikishwa darasa la 6 katika maeneo sita ya muda ya kujifunzia yaliyoanzishwa na UNICEF karibu na kambi ya wakimbizi wa ndani ya Rusayo jimboni Kivu Kaskazini nchini DRC.
Asifiwe Bihamera na binti yake Timi, mwenye umri wa miaka 3, ambaye aliambukizwa kipindupindu. Anapatiwa matibabu kitu cha afya ya Buhimba Aleluya karibu na Goma, jimboni Kivu Kaskazini.
Céline, mwenye umri wa miaka 4 mkazi wa jimbo la Kwango nchini DRC, amepatiwa chanjo dhidi ya polio na hapo anawekewa alama kidoleni kuthibitisha amechanjwai. Mdogo wake wa kiume naye pia alipatiwa chanjo hiyo.
Mfanyakazi wa UNICEF akikagua vifaa ikiwemo dawa, vidonge vya kusafisha maji, na maboza ya baada ya kuwasilii Goma ,Kivu Kaskazini kama sehemu ya hatua dhidi ya kipindupindu mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
UNICEF kupitia fedha za mfuko wa dharura wa Umoja wa Mataifa, CERF umeanzisha maeneo ya kujifunzia ya dharura ya muda katika kambi za wakimbizi. UNICEF pia inagawa vifaa vya shule, kama vile mabegi ya kubebea madaftari.
Mwenye kizibao cha buluu ni Uwezo, mtoto mkimbizi mwenye umri wa miaka 11 akicheza soka na watoto wengine kwenye kituo rafiki cha watoto kilichoandaliwa na UNICEF na wadau kwenye eneo la Nyiragongo, kaskazini mwa mji wa Goma, jimboni Kivu Kaskazini, DRC.