Mafuriko yaliyosababishwa na kujaa kwa maji Ziwa Tanganyika yafurusha watu Burundi, IOM yasaidia
Shirika la Umoja wa Mataifa la Uhamiaji, IOM na wadau wake wa masuala ya kibinadamu wamesambaza misaada ya dharura kwa familia za watu ambao wamelazimika kukimbia makwao kutokana na mafuriko yaliyosababishwa na kuongezeka kwa kina cha maji cha Ziwa Tanganyika na mto Rusizi.