UNICEF Burundi yatoa mafunzo ya Ujuzi kwa wasichana
Shirika la umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF linaendesha programu maalumu ya mafunzo kwa wasichana nchini Burundi kwa lengo la kupunguza pengo la wanawake kwenye sayansi na stadi za kazi ambapo wahitimu arobaini kutoka majimbo manne wamepatiwa vyeti vya kuhitimu.