Ujumbe wa Katibu Mkuu wa UN kwa viongozi: ‘Amkeni, badilisheni mwelekeo, unganeni’
Katika mahojiano maalum na Idhaa ya Umoja wa Mataifa, UN News, iliyogusa maeneo mbalimbali, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres anatoa wito kwa viongozi duniani ‘waamke’ wabadili mwelekeo na wachukue mwelekeo sahihi nyumbani kwao na duniani na waungane.