Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Burundi

Watoto wakiteka maji machafu katika mto karibu na nyumbani jimbo la Ruyigi nchini Burundi. Septemba 14, 2017
© UNICEF/UN0185046/Haro

Licha ya ahadi, Burundi yaendelea kukiuka haki za binadamu na kufunga malngo wa demokrasia: HRC

Tume ya Umoja wa Mataifa ya uchunguzi kuhusu hali ya haki za binadamu nchini Burundi imesema licha ya ahadi za awali za Rais Évariste Ndayishimiye za kuboresha haki za binadamu nchini mwake na kurejesha utawala wa sheria, bado hakuna hatua zozote zilizochukuliwa kutimiza ahadi hizo, huku jukwaa la kidemokrasia likiendelea kufungwa na ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu ukitamalaki tangu Rais huyo achukue madaraka Juni 2020.

Sauti
3'32"
Mkimbizi wa ndani nchini Msumbiji akipokea msaada wa chakula
© WFP/Grant Lee Neuenburg

Kuisaidia WFP ni kuwasaidia wakimbizi kama Adu

Mkimbizi wa ndani Abbas Adu na wengine 400,000 wamelishukuru Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa chakula WFP kuwapatia msaada wa chakula wakati huu ambapo WFP imepaza sauti kwa wahisani kusaidia wananchi Milioni 41 wanaokabiliwa na njaa kutokana na hali mbaya ya hewa ambayo imeathiri mavuno yao na hivyo kukosa chakula.

Sauti
2'2"
Msanii akichora picha kwenye ukuta jinsi ya mbinu za mtu kujikinga dhidi ya virusi vya COVID-1 nchini Jamhuri ya afrika ya kati, CAR..
MINUSCA/Screenshot

Nchi za Afrika ya Kati zimedhibiti vyema COVID-19-UN

Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika ukanda wa Afrika ya Kati François Louncény Fall amehutubia Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa na kusema kuwa harakati za serikali kwenye ukanda huo pamoja na wadau wao kukabili janga la ugonjwa wa Corona au COVID-19 zimewezesha ukanda huo kuwa wenye idadi ndogo zaidi ya wagonjwa na vifo vitokanavyo na ugonjwa huo barani Afrika.