Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Burundi

Familia kutoka Eritrea ikiwa kwenye kituo cha muda Romani wakisubiriwa kuhamishwa hadi Netherlands.
© UNHCR/Stefan Lorint

Idadi ya wasaka hifadhi nchi ya tatu kuongezeka 2023

Zaidi ya wakimbizi milioni 2 mwaka ujao WA 2023 watahitaji kuhamishiwa nchi ya tatu ikiwa ni ongezeko kwa asilimia 36 ikilinganishwa na mahitaji ya mwaka huu ambayo ni wakimbizi milioni 1.5 pekee, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR kupitia tathmini ya makadirio ya kuhamia nchi ya tatu kwa mwaka 2022.

Vital Bambanze (kulia) mwakilishi wa jamii ya watwa nchini Burundi akiwa kwenye majadiliano na washiriki wengine wakati wa mkutano wa 21 wa jukwaa la Kudumu la Umoja wa Mataifa la watu wa asili, UNPFII mwezi Aprili 2022 jijini New York, Marekani.
UN/ Flora Nducha

Nuru Burundi kwa haki za jamii ya Watwa

Mkutano wa 21 wa Jukwaa la Kudumu la Umoja wa Mataifa la watu wa asili, UNPFFII likiwa limeingia siku ya tatu kwenye makao makuu ya Umoja huo jijini New York, Marekani, washiriki kutoka Burundi wameieleza Idhaa ya Kiswahili ya  Umoja wa Mataifa juu ya hatua zinazoendelea kuchukuliwa ili kuhakikisha haki za binadamu za jamii ya asili aina ya watwa zinazingatiwa.
 

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres (kushoto) na Rais Samia Suluhu Hassan wa Tanzania baada ya mazungumzo jijini New York, Marekani.mwezi Septemba 2021 (Maktaba)
UN / Evan Schneider

Tumeomba mazungumzo na UN wasaidie hali Burundi ili kuandaa Tanzania  kuwarejesha wakimbizi - Rais Samia 

Tanzania ni moja ya nchi za Afrika mashariki ambazo zimekuwa kimbilio la wakimbizi kwa miaka mingi. Rais wa nchi hiyo Samia Suluhu Hassan alipozungumza na Idhaa hii ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa alipokuwa hapa New York, Marekani anasema ni takribani miaka 50 kwa nyakati tofauti nchi yake imekuwa ikipokea wakimbizi na kwa sasa ameomba mazungumzo na mashirika ya Umoja wa Mataifa likiwemo la kuhudumia wakimbizi UNHCR kusaidia katika nchi wanakotoka wakimbizi ili waweze kurejea akitolea mfano Burundi.

Sauti
2'57"
Maza, ng'ombe ambaye amebadili maisha ya familia maskini nchini Burundi
@UNICEFBurundi/2021/Hamburger

Ng’ombe mmoja aleta hakikisho la maisha kwa kaya maskini Burundi

Mtamba mmoja wa ng’ombe anaweza kuonekana si chochote kitu kwa wafugaji wabobezi lakini kwa Beatrice Nibogora na familia yake nchini Burundi, mtamba huyo akipatiwa jina Maza amegeuka lulu na ufunguo wa maisha yenye matumaini na kutimiza methali ya wahenga ya kwamba baada ya dhiki ni faraja. Hii ni baada ya mradi wa Benki ya Dunia na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF kubisha hodi kunusuru kaya maskini.

Sauti
1'58"