Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Burundi

Watoto wakimbizi kutoka Somalia wakiwa kwenye kambi ya wakimbizi ya Daadab nchini Kenya ambako WFP inawapatia misaada ya dharura.
WFP/Rose Ogola

Majanga yanavyozidi kushamiri isiwe kisingizio cha kusigina haki za mtoto- UN

Wataalamu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa hususan zile za mtoto wametoa taarifa ya pamoja hii leo huko Geneva, Uswisi wakisema  majanga ya kiafya, kibinadamu na yale  yanayohusiana na tabianchi yakizidi kuongeza changamoto kubwa duniani kila uchao kama vile ukimbizi wa ndani, ukatili wa kingono na njaa, serikali lazima zikumbuke kuwa watoto wana haki kamilifu za kimsingi za kibinadamu na kwamba haki hizo zinapaswa kulindwa.

Watoto wakimbizi wa ndani huko Ituri nchini DRC.
UN/Eskinder Debebe

Mauaji na utekaji nyara wa watoto kwenye maeneo ya vita vilishamiri mwaka 2021- Ripoti

Mwaka wa 2021  umeshuhudia mchanganyiko wa mwendelezo hatari wa mizozo, mapinduzi ya kijeshi sambamba na mizozo mipya na ile iliyodumu muda mrefu na ukiukwaji mkubwa wa sheria za kimataifa, vyote ambavyo kwa pamoja vimekuwa na madhara makubwa kwa watoto duniani kote, amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kupitia ripoti yake ya mwaka kuhusu Watoto kwenye mizozo ya kivta, ripoti ambayo imechapishwa hii leo.