Ripoti yafichua jinsi watu wanabinywa wasishirikiane na UN kulinda haki
Watu katika mataifa 42 duniani kote wanakabiliwa na kulipiziwa visasi na vitisho kutokana na ushirikiano wao na Umoja wa Mataifa kuhusu masuala ya haki za binadamu, imesema ripoti ya mwaka ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa iliyowasilishwa leo na msaidizi wake mbele ya Baraza la Umoja wa Mataifa la haki za binadamu.