UNGA80
EAC yasisitiza usalama, uchumi na masuala ya kidijitali katika Mjadala Mkuu wa UNGA80
Kama unavyofahamu Mjadala Mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa UNGA80 umekunja jamvi rasmi jana Jumatatu. Na tumepata fursa ya kuzungumza na washiriki mbalimbali akiwemo Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki EAC, Veronica Nduva ambaye alizungumza na Flora Nducha kandoni mwa mjadala huo kuangazia mchango wa Jumuiya ya Afrika Mashariki katika kutekeleza ajenda ya Umoja wa Mataifa ikiwemo masuala ya Amani na usalama, maendeleo na ushirikiano wa kikanda. Ungana nao.
EAC yasisitiza usalama, uchumi na masuala ya kidijitali katika UNGA80
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki EAC, Veronica Nduva, akizungumza na Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa ameeleza jinsi jumuiya hiyo inavyoshirikiana na mashirika ya kikanda na kimataifa kuhakikisha usalama katika maeneo yenye mizozo ya kisiasa na mipaka ya nchi wanachama.
30 SEPTEMBA 2025
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayomulika ujumbe wa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki EAC, Veronica Nduva ambaye alizungumza na Flora Nducha kandoni mwa UNGA80. Pia tunakuletea muhtasari wa habari kama zifuatazo.
Viongozi wa UN na wadau kumulika zahma inayokabili wakimbizi wa kabila la warohingya
Zaidi ya miaka minane tangu zaidi ya wakimbizi 750,000 waislamu wa kabila la warohingya wakimbie Myanmar kuelekea kwenye kambi kubwa nchini Bangladesh, mgogoro huo bado haujapatiwa suluhisho