Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNGA80

Mkutano wa Baraza Kuu - Taarifa Maalum ya UNGA80
23 Septemba – 30 Septemba 2025
Jukwaa limewekwa tayari kwa ajili ya Mjadala Mkuu wa Mkutano wa 80 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.
Mkutano huu utafunguliwa chini ya kaulimbiu “Bora Pamoja: Miaka 80 na Zaidi kwa Amani, Maendeleo na Haki za Binadamu”, ikiwa ni hatua muhimu inayofanyika katikati ya changamoto kubwa duniani na wito wa dharura wa kuchukua hatua mpya za ushirikiano wa kimataifa.
Mjadala wa Ngazi ya Juu utaanza rasmi tarehe 22 Septemba kwa siku nzima ya mikutano ya kilele na maadhimisho, ikiwemo kumbukumbu ya miaka 80 tangu kuanzishwa kwa Umoja wa Mataifa, tukio la wakati wa Malengo ya Maendeleo Endelevu au SDG Moment na kutimia miaka 30 tangu Mkutano wa Dunia wa Beijing kuhusu wanawake. Viongozi pia watashiriki kwenye mkutano wa ngazi ya juu kuhusu Suluhu ya amani kwa suala la Palestina na utekelezaji wa suluhu ya mataifa mawili.
Kuanzia tarehe 23 hadi 29 Septemba, macho na masikio ya dunia yatageukia jukwaa maarufu lenye marumaru ya kijani ndani ya Ukumbi wa Baraza Kuu, ambapo marais, mawaziri wakuu na wafalme watawasilisha taarifa za kitaifa, wakibainisha dira zao kuhusu amani, maendeleo, haki za binadamu na hatua za pamoja wakati huu wa changamoto zinazoongezeka duniani.
Ajenda pia itahusisha mkutano wa kilele unaofanyika kila baada ya miaka miwili kuhusu ufadhili wa maendeleo endelevu, Mkutano wa Tabianchi, uzinduzi wa Mazungumzo ya kimataifa kuhusu Usimamizi wa Akili Mnemba AI, Hatua za dunia kuhusu magonjwa yasiyoambukiza NDCs na afya ya akili, pamoja na hali ya Waislamu Warohingya na wengine walio wachache nchini Myanmar.
Hapa, Idhaa ya Kiswahili inakupa fursa ya kuketi mstari wa mbele kushuhudia yote yanayojiri. Kupitia simu yako ya rununu au kompyuta, fuatilia Wakuu wa Nchi na Serikali wanapojadili masuala makubwa ya wakati wetu na kuelekeza dira ya taswira mpya ya Umoja wa Mataifa.
 
Tembelea majukwaa yetu ya mitandao ya kijamii: Youtube: Habari za UN X: Habari za UN
Edouard Bizimana, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kikanda wa Burundi, akihutubia mjadala mkuu wa mkutano wa 80 wa Baraza Kuu la UN.
UN Photo/Loey Felipe

Burundi imefunga ukusara wa machafuko na kufungua wa maridhiano: Bizimana

Katika hotuba yenye nguvu katika kikao cha 80 cha Mjadala Mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA80 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kikanda wa Burundi, Balozi Edouard Bizimana, amethibitisha ahadi ya nchi yake kwa suala la  amani, maendeleo, na haki za binadamu huku akiutaka Umoja wa Mataifa kufanya marekebisho ya dharura ili kuendana na changamoto za dunia ya sasa. Akimwakilisha Rais Evariste Ndayishimiye, Bizimana amesisitiza nafasi muhimu ya ushirikiano wa kimataifa katika kukabiliana na migogoro ya kidunia.

Mkurugenzi Mkuu wa ECSA - HC, Dkt. Ntuli Kiapologwe akizungumza na Anold Kayanda wa Idhaa ya Umoja wa Mataifa katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani, Septemba 2025.
UN News

Ili Afrika ‘iimarike kiafya’ inabidi isiwe tegemezi kwenye masuala ya kifedha - Dkt. Ntuli Kapologwe

Tukisalia hapa katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa, kandoni mwa Mjadala Mkuu wa Mkutano wa 80 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA80, inafanyika mikutano mingine ya pembezoni kujadili masula mengine ya kusongesha maendeleo ya ulimwengu. Wiki iliyopita tulizungumza na Dkt. Ntuli Kapologwe Mkurugenzi Mkuu wa Jumuiya ya Afya ya Mashariki, Kati na Kusini mwa Afrika, ECSA wakati alipokuwa akisubiri kushiriki mkutano  wa nchi wanachama wa jumuiya hiyo kujadili jinsi ya kusongesha diplomasia ya kisayansi ili kuhakikisha bara la Afrika haliachwi nyuma kwenye kukabiliana na changamoto za kiafya.

Sauti
3'29"
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres akihutubia sehemu ya ufunguzi wa Mjadala Mkuu wa UNGA80 New York, Marekani Septemba 23, 2025
UN Photo/Loey Felipe

NUKUU ZA VIONGOZI: Mjadala Mkuu wa Baraza Kuu la UN, UNGA80- SIKU YA SITA

Mjadala Mkuu wa mkutano wa 80 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa leo ni siku ya sita ambapo viongozi wa dunia wanaendelea kutoa hotuba zao kwenye ukumbi wa Baraza Kuu kuhusu yale waliyofanya kusongesha amani, haki za binadamu na maendeleo duniani. Kila kiongozi wa nchi 193 wanachama wa Umoja wa Matiafa atapata fursa ya kuhutubia kwenye mjadala huo utakaofikia tamati tarehe 29 Septemba. Bofya hapa kupata ratiba. Mjadala huanza saa 3 asubuhi kwa saa za New York, Marekani hadi saa 3 usiku. Tazama Mubashara hapa

Kando ya hotuba hizo, wanashiriki vikao vya kando vinavyomulika masuala kama vile afya,  amani na usalama duniani.