UNGA80
Kinachohitajika ni biashara tujitegemee na si misaada- Rwanda
- Tushirikiane UN ikidhi mahitaji ya sasa
- Biashara badala ya misaada
- Tunaunga mkono marekebisho ya UN
- Tuko tayari kupokea ofisi za mashirika ya UN
Sudan Kusini: Wafadhili wa tabianchi timizeni ahadi zenu
Pamoja na kuwa nchi ya Sudan Kusini inachangia kwa kiasi kidogo kwenye uharibifu wa tabaka la ozoni lakini taifa hilo changa duniani linaendelea kuathirika kwa kiasi kikubwa na athari za mabadiliko ya tabianchi na kuwaacha wananchi wakiteseka.
Haiti: Kiongozi wa mpito atoa wito wa hatua za haraka za kimataifa kukabili mgogoro wa usalama
Rais wa Baraza la Rais la Mpito la Haiti, Anthony Franck Laurent Saint Cyr, ametoa wito mbele ya Mjadala Mkuu waBaraza Kuu la Umoja wa Mataifa, akionya kwamba Haiti iko katikati ya tishio kubwa la kiusalama la kikanda na ametaka hatua za haraka na za pamoja za kimataifa zichukuliwe kuinusuru.
Mfalme Mswati III apendekeza Kamati Maalum za muda ili kutatua migogoro ya kimataifa
Akihutubia Mjadala Mkuu wa Mkutano wa 80 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, jijini New York, Marekani Alhamisi ya Septemba 25, Mfalme Mswati III wa Eswatini ametoa wito wa kuundwa kwa kamati maalum za muda ili kushughulikia migogoro ya kimataifa.
Hakuna amani kama hakuna haki na hakuna haki kama Palestina haiko huru: Abbas
Rais wa Palestina, Mahmoud Abbas, leo amehutubia Mjadala Mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa UNGA80 kwa njia ya video baada ya Marekani kushindwa kumpa visa ya kuingia nchini humo.
Somalia: Afrika haiwezi kuachwa nje tena ni wakati wa kuwa na usawa wa kimtazamo duniani
Rais wa Somalia, Hassan Sheikh Mohamud, ametoa hotuba yenye uzito mkubwa kwenye Mjadala Mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa UNGA80 hii leo akitaka nchi wanachama kujitolea upya kwa misingi ya usawa, mshikamano na ushirikiano wa kimataifa.
25 SEPTEMBA 2025
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina maalum inayomulika mkutano wa ngazi ya juu kuhusu magonjwa yasiyo ya kuambukiza NDCs unaoendelea kandoni mwa UNGA80, na tumezungumza na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa WHO Kanda ya Afrika Dkt. Mohamed Yakub Janabi.