UNGA80
Comoro yaitaka dunia kuchukua hatua kuhusu Palestina, ikisema kisasi cha Israel ni mauaji ya kimbari
Akihutubia viongozi wa dunia katika kikao cha 80 cha Mjadala Mkuu wa Umoja wa Mataifa UNGA80, Rais Azali Assoumani wa Muungano wa Comoros ameonya kuwa binadamu wanazidi kupotea kutoka kwenye dira ya amani na haki iliyoahidiwa na Malengo ya Maendeleo Endelevu.
Namibia ni simulizi ya mafanikio makubwa zaidi ya UN - Rais Netumbo
Rais Netumbo Nandi-Indaitwa wa Namibia amehutubia Mjadala Mkuu wa Mkutano wa 80 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, (UNGA80) jijini New York Marekani ambapo pamoja na mambo mengine amesihi jamii ya kimataifa kutambua mchango wa wanawake na wanaume wanaohudumu chini ya bendera ya buluu ya Umoja wa Mataifa wakihaha huku na kule kusongesha amani.
Mdahalo wa IA: Hatuwezi kuacha hatima ya binadamu iamuliwe na algorithimu
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limefanya mdahalo wa wazi wa ngazi ya juu mada ikiwa ni“Akili mnemba na amani na usalama wa kimataifa” chini ya ajenda ya “Uendelezaji wa amani na usalama wa kimataifa.”
Nchi zaweka bayana ahadi na hatua zinazochukua kukabilii mabadiliko ya tabianchi
Viongozi kutoka zaidi ya nchi 100 wametangaza ahadi zao au kile ambacho wanatekeleza kuhakikisha kwamba wanakabiliana na madhara ya mabadiliko ya tabiachi. Hatua kuanza kutumia nishati safi na salama hali kadhalika kupanda miti.
Nini kilisababisha kukwama kwa eskaleta aliyokuwa amepanda Rais wa Marekani Donald Trump UN?
Umoja wa Mataifa umetoa taarifa rasmi kuhusu tukio lililomhusisha Rais wa Marekani, Donald Trump, katika moja ya eskaleta kwenye Makao Makuu ya Umoja huo alipowasili Jumanne asubuhi ili kuhutubia Mjadala Mkuu wa Baraza Kuu la chombo hicho.
ITU, Will.i.am, na Google wazindua mafunzo ya AI na roboti kwa vijana barani Afrika
Shirika la Umoja wa Mataifa la Muungano wa Mawasiliano ITU linalohusika na teknolojia za kidijitali, limeungana na mjasiriamali wa teknolojia na mwanamuziki nyota will.i.am pamoja na kampuni ya Google ili kutoa mafunzo ya Akili mnemba AI na roboti kwa wanafunzi barani Afrika.
Guterres awasihi viongozi kufanikisha ufadhili kwa ajili ya mustakabali imara, jumuishi na endelevu
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amefungua Mkutano wa kwanza wa kila miaka miwili wa Uchumi Endelevu, Jumuishi na Imara kwa wito wa kuchukua hatua thabiti ili kurekebisha mifumo ya kifedha ya kimataifa na kuziba pengo la maendeleo linaloongezeka.
Ukraine: Taasisi za kimataifa zimekuwa dhaifu
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskyy amesema taasisi za kimataifa zimekuwa dhaifu wanachoweza kufanya ni kutoa matamko makali pekee na kwamba kwa sasa duniani sheria pekee za Kimataifa haziwezi kusaidia nchi kujilinda bila ya kuwa na silaha pamoja na marafiki wenye nguvu wa kukusaidia.
Taasisi za kimataifa zimekuwa dhaifu - Volodymyr Zelenskyy
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskyy amesema taasisi za kimataifa zimekuwa dhaifu wanachoweza kufanya ni kutoa matamko makali pekee na kwamba kwa sasa duniani sheria pekee za Kimataifa haziwezi kusaidia nchi kujilinda bila ya kuwa na silaha pamoja na marafiki wenye nguvu wa kukusaidia. Tupate taarifa zaidi kutoka kwa Leah Mushi.
ECSA: Diplomasia ya kisayansi kutumika kusongesha Mkataba wa Zama Zijazo Afrika
Katika siku ya pili ya Mjadala Mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA, kando ya hotuba, viongozi wa nchi 9 wanachama wa Jumuiya ya Afya ya Mashariki, Kati na Kusini mwa Afrika, ECSA watakuwa na mkutano wa kusongesha diplomasia ya kisayansi ili kuhakikisha bara la Afrika haliachwi nyuma kwenye kukabiliana na changamoto za kiafya, baada ya kujifunza kutokana na COVID-19 au UVIKO19. Mkurugenzi Mkuu wa ECSA Dkt. Ntuli Kapologwe akihojiwa na Assumpta Massoi wa Idhaa hii ametaja wanachotarajia kwenye mkutano huo..
Pagination
- 1
- 2