UNGA80
Akiwa Doha, Rais wa Baraza Kuu aona watoto wa kipalestina walivyo na matumaini licha ya zahma walizopita
Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Annalena Baerbock ametembelea wakimbizi wa kipalestina huko Doha nchini Qatar kuwajulia hali na kujionea maisha yao baada ya kuondolewa wakati wa vita kali huko Ukanda wa Gaza eneo la wapalestina linalokaliwa kimabavu na Israel na kuletwa nchini Qatar kwa ajili ya kupatiwa matibabu. Leah Mushi anatupa taswira ya ziara yake hiyo.
Namna UNCDF ilivyosaidia jamii kupata mtaji na huduma muhimu Rwanda, Burundi, Malawi na Zimbabwe
Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuendeleza Mitaji, UNCDF, limeendelea kuwekeza katika kupunguza hatari za hasara za kifedha na kufungua fursa za mitaji nafuu kwa vijana, wanawake na sekta muhimu barani Afrika. Hayo yanasemwa na Omon Ukpoma-Olaiya, Kiongozi wa Uwekezaji wa UNCDF kwa Kanda ya Afrika Mashariki, Kusini na Nchi za Kiarabu, alipokuwa akizungumza na Anold Kayanda na Anold Kayanda wa Idhaa ya Umoja wa Mataifa, jijini New York, Marekani kandoni mwa Mjadala Mkuu wa Mkutano wa 80 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa uliofikia tamati Septemba 29, 2025.
Takwimu za UNGA: Hotuba ndefu zaidi, Wanawake Wachache, na baadhi kutokuwepo
Kwa muda wa siku sita, safu ya viongozi wa dunia (194 kwa jumla, 24 tu kati yao wakiwa ni wanawake) walitoa hotuba kwenye Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kutoka kwenye jukwaa lake la kuvutia la marumaru ya kijani kibichi, wakiangazia vita huko Jamhuri ya Kidemokrasia Congo, DRC, Sudan, Gaza na Ukraine, mzozo wa mabadiliko ya tabianchi, na mageuzi katika Umoja wa Mataifa, miongoni mwa masuala mengine mengi muhimu.
EAC yasisitiza usalama, uchumi na masuala ya kidijitali katika Mjadala Mkuu wa UNGA80
Kama unavyofahamu Mjadala Mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa UNGA80 umekunja jamvi rasmi jana Jumatatu. Na tumepata fursa ya kuzungumza na washiriki mbalimbali akiwemo Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki EAC, Veronica Nduva ambaye alizungumza na Flora Nducha kandoni mwa mjadala huo kuangazia mchango wa Jumuiya ya Afrika Mashariki katika kutekeleza ajenda ya Umoja wa Mataifa ikiwemo masuala ya Amani na usalama, maendeleo na ushirikiano wa kikanda. Ungana nao.
EAC yasisitiza usalama, uchumi na masuala ya kidijitali katika UNGA80
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki EAC, Veronica Nduva, akizungumza na Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa ameeleza jinsi jumuiya hiyo inavyoshirikiana na mashirika ya kikanda na kimataifa kuhakikisha usalama katika maeneo yenye mizozo ya kisiasa na mipaka ya nchi wanachama.
30 SEPTEMBA 2025
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina inayomulika ujumbe wa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki EAC, Veronica Nduva ambaye alizungumza na Flora Nducha kandoni mwa UNGA80. Pia tunakuletea muhtasari wa habari kama zifuatazo.
Viongozi wa UN na wadau kumulika zahma inayokabili wakimbizi wa kabila la warohingya
Zaidi ya miaka minane tangu zaidi ya wakimbizi 750,000 waislamu wa kabila la warohingya wakimbie Myanmar kuelekea kwenye kambi kubwa nchini Bangladesh, mgogoro huo bado haujapatiwa suluhisho
Pazia la Mjadala Mkuu UNGA80 lafungwa kwa wito wa uwiano wa uwakilishi, mageuzi na hatua za pamoja
Siku sita za Mjadala Mkuu wa Mkutano wa 80 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UNGA80) zimetamatika leo Jumatatu Septemba 29 alasiri kwa Rais wa Baraza hilo Annalena Baerbock kuhutubia na kusisitiza umuhimu wa uwakilishi wa kimataifa, mshikamano, na kasi ya kufanyia mageuzi chombo hicho katika dunia inayobadilika kwa kasi.
Vatican yasisitiza amani, upokonyaji silaha na heshima kwa ubinadamu: UNGA80
Vaticani ametoa wito mzito wa mshikamano wa kimataifa, amani na haki wakati wa Mjadala Mkuu wa Mkutano wa 80 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, ambapo Askofu Mkuu Paul Richard Gallagher, Katibu wa Uhusiano na Mataifa wa Vatican, ameonya kuwa dunia ipo katika njia panda ya hatari.
Malawi: Ushiriki wa wanawake katika operesheni za ulinzi wa amani ‘unalipa’
Malawi katika Mjadala Mkuu wa mkutano wa 80 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa imewakilishwa na Balozi Agnes Mary Chimbiri-Molande ambaye amezungumzia maendeleo ambayo nchi yake imepiga katika kukuza usawa wa kijinsia na ushiriki wa wanawake katika operesheni za ulinzi wa amani.