UNGA80
Uhaba wa maji watishia mafanikio ya SDGs – Guterres
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, ameonya kwamba dunia ipo nyuma katika kutekeleza ahadi zake kuhusu upatikanaji wa maji safi na salama na huduma za kujisafi. Hivyo basi amezitaka serikali, sekta binafsi na jamii kuchukua hatua za haraka kukabiliana na uhaba unaoongezeka wa maji, uchafuzi wa mazingira na shinikizo linalotokana na mabadiliko ya tabianchi. Assumpta Massoi na maelezo zaidi.
Kutoka Akili Mnemba (AI) hadi ‘roboti zinazoua: Guterres ataka mfumo wa kuisimamia
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, amesema ni lazima kuweko kwa udhibiti mpana wa kimataifa wa akili mnemba au (AI) wakati huu ambapo chipu za AI zenye uwezo mkubwa ambazo zilibuniwa kwa matumizi ya kiraia zinaanza kutumika vitani, ambako “roboti za kuua” tayari zinatumika.
01 JULAI 2026
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina. Ikiwa ni siku chache baada ya maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Watu Wasioona na viziwi inayoadhimishwa tarehe 27 Juni kila mwaka, Rashid Malekela wa Idhaa hii anakupeleka Mashariki ya Kati akimmulika mkazi mwenye ulemavu ambaye anakumbwa na changamoto katikati ya vita.
UN yaondoa kanuni ya kifedha iliyoutaka kurejesha fedha hata kama haijazipokea
- Kanuni ilikwamisha ajira na operesheni za ulinzi wa amani
- Fedha zilizurejeshwa bila hata kupokelewa
- Nchi wanachama zilihamishia fedha hizo bajeti ya mwaka ufuatao
- Mwaka 2025 bajeti ilikuwa na nakisi ya dola bilioni 1.6 za michango isiyolipwa
23 APRILI 2026
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambapo juzi Jumanne na jana Jumatano wagombea wa nafasi ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa walipata fursa kunadi serra zao mbele ya nchi wanachama kwenye Baraza Kuu wakiwemo wawakilishi wa asasi za kiraia walioweza kuwauliza maswali.
Miongoni mwa wawakilishi hao ni Irene Kitoti, Mwanzilishi na mkurugenzi wa asasi ya kiraia ya Genesis For Children Organization ya nchini Tanzania aliyezungumza na Flora Nducha wa Idhaa hii ya Kiswahili. Pia tunakuletea muhtasari wa habari kama zifuatazo.
UN yatoa wito mpya wa kukomesha ukoloni huku maeneo 17 yakiwa bado chini ya utawala wa kigeni
Je wajua kuwa hadi sasa kuna maeneo 17 duniani yanatawaliwa, yaani bado yanakabiliwa na ukoloni? Ni kwa mantiki hiyo hii leo Umoja wa Mataifa umetoa wito mpya wa kukomesha ukoloni, ukionya kuwa maeneo 17 yasiyojitawala bado yako chini ya usimamizi wa mataifa ya kigeni.
Akiwa Doha, Rais wa Baraza Kuu aona watoto wa kipalestina walivyo na matumaini licha ya zahma walizopita
Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Annalena Baerbock ametembelea wakimbizi wa kipalestina huko Doha nchini Qatar kuwajulia hali na kujionea maisha yao baada ya kuondolewa wakati wa vita kali huko Ukanda wa Gaza eneo la wapalestina linalokaliwa kimabavu na Israel na kuletwa nchini Qatar kwa ajili ya kupatiwa matibabu. Leah Mushi anatupa taswira ya ziara yake hiyo.
Namna UNCDF ilivyosaidia jamii kupata mtaji na huduma muhimu Rwanda, Burundi, Malawi na Zimbabwe
Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuendeleza Mitaji, UNCDF, limeendelea kuwekeza katika kupunguza hatari za hasara za kifedha na kufungua fursa za mitaji nafuu kwa vijana, wanawake na sekta muhimu barani Afrika. Hayo yanasemwa na Omon Ukpoma-Olaiya, Kiongozi wa Uwekezaji wa UNCDF kwa Kanda ya Afrika Mashariki, Kusini na Nchi za Kiarabu, alipokuwa akizungumza na Anold Kayanda na Anold Kayanda wa Idhaa ya Umoja wa Mataifa, jijini New York, Marekani kandoni mwa Mjadala Mkuu wa Mkutano wa 80 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa uliofikia tamati Septemba 29, 2025.
Takwimu za UNGA: Hotuba ndefu zaidi, Wanawake Wachache, na baadhi kutokuwepo
Kwa muda wa siku sita, safu ya viongozi wa dunia (194 kwa jumla, 24 tu kati yao wakiwa ni wanawake) walitoa hotuba kwenye Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kutoka kwenye jukwaa lake la kuvutia la marumaru ya kijani kibichi, wakiangazia vita huko Jamhuri ya Kidemokrasia Congo, DRC, Sudan, Gaza na Ukraine, mzozo wa mabadiliko ya tabianchi, na mageuzi katika Umoja wa Mataifa, miongoni mwa masuala mengine mengi muhimu.
EAC yasisitiza usalama, uchumi na masuala ya kidijitali katika Mjadala Mkuu wa UNGA80
Kama unavyofahamu Mjadala Mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa UNGA80 umekunja jamvi rasmi jana Jumatatu. Na tumepata fursa ya kuzungumza na washiriki mbalimbali akiwemo Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki EAC, Veronica Nduva ambaye alizungumza na Flora Nducha kandoni mwa mjadala huo kuangazia mchango wa Jumuiya ya Afrika Mashariki katika kutekeleza ajenda ya Umoja wa Mataifa ikiwemo masuala ya Amani na usalama, maendeleo na ushirikiano wa kikanda. Ungana nao.