Mkutano wa 76 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, #UNGA76 umefunguliwa Jumanne ya tarehe 14 mwezi Septemba mwaka 2021 kwenye makao makuu jijini New York, Marekani. Mjadala Mkuu wa ngazi ya juu utaanza Jumanne ya tarehe 21 mwezi Septemba mwaka 2021 na kumalizika tarehe 27 mwezi Septemba 2021. Katika ukurasa huu utapata taarifa motomoto kuhusu mjadala huo mkuu wa ngazi ya juu na matukio mengine ikiwemo miaka ufadhili kwa ajili ya mabadiliko ya tabianchi, mifumo ya chakula, maadhimisho ya miaka 20 ya azimio la Durban linalopinga ubaguzi wa rangi na ubaguzi wa aina zingine zote, mabadiliko ya tabianchi na ulinzi na usalama, masuala ya nishati na pia kuenziwa kwa aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Dag Hammarskjöld.Vikao vingine vya ngazi ya juu vitakavyofanyika wakati wa wiki za mwanzo za #UNGA76 ni pamoja na mkutano wa ngazi ya juu kuhusu COVID-19. UNGA76 inafanyika wakati janga la COVID-19 likiendelea kwa hiyo vikao vitafanyika moja kwa moja ukumbini makao makuu ya Umoja wa Mataifa lakini pia kwa njia ya mtandao ambapo baajhi ya wakuu wa nchi na serikali hotuba zao zitakuwa kititolewa kwa njia ya mtandao.
Tufuatilie katika majukwaa yetu ya mtandao wa kijamii
YouTube: https://www.youtube.com/c/UNNewsKiswahili
Twitter: https://twitter.com/HabarizaUN