Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNGA 76 using tag UNGA76

MKUTANO WA 76 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA
21 Septemba 2021-27 Septemba 2021

Mkutano wa 76 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, #UNGA76 umefunguliwa Jumanne ya tarehe 14 mwezi Septemba mwaka 2021 kwenye makao makuu jijini New  York, Marekani. Mjadala Mkuu wa ngazi ya juu utaanza Jumanne ya tarehe 21 mwezi Septemba mwaka 2021 na kumalizika tarehe 27 mwezi Septemba 2021. Katika ukurasa huu utapata taarifa motomoto kuhusu mjadala huo mkuu wa ngazi ya juu na matukio mengine ikiwemo miaka ufadhili kwa ajili ya mabadiliko ya tabianchi, mifumo ya chakula, maadhimisho ya miaka 20 ya azimio la Durban linalopinga ubaguzi wa rangi na ubaguzi wa aina zingine zote, mabadiliko ya tabianchi na ulinzi na usalama, masuala ya nishati  na pia kuenziwa kwa aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Dag Hammarskjöld.Vikao vingine vya ngazi ya juu vitakavyofanyika wakati wa wiki za mwanzo za #UNGA76 ni pamoja na mkutano wa ngazi ya juu kuhusu COVID-19.  UNGA76 inafanyika wakati  janga la COVID-19 likiendelea kwa hiyo vikao vitafanyika moja kwa moja ukumbini makao makuu ya Umoja wa Mataifa lakini pia kwa njia ya mtandao ambapo baajhi ya wakuu wa nchi na serikali hotuba zao zitakuwa kititolewa kwa njia ya mtandao.

Tufuatilie katika majukwaa yetu ya mtandao wa kijamii

YouTube: https://www.youtube.com/c/UNNewsKiswahili

Twitter: https://twitter.com/HabarizaUN

Jarida 24 Septemba 2021

Ni Ijumaa ya tarehe 24 mwezi Septemba mwaka 2021 karibu kusikiliza jarida na kama ilivyo ada ya kila Ijumaa tunakuletea mada kwa kina ambapo leo tunakuletea sehemu ndogo ya mahojiano marefu na Rais Samia Suluhu Hassan wa Tanzania baada ya hapo jana kuhutubia kwa mara yake ya kwanza katika Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa. 

Sauti
12'6"

Jarida 23 Septemba 2021

Ni Alhamisi  ya tarehe 23  ya mwezi Septemba mwaka 2021 siku ya tatu ya mjadala mkuu wa mikutano ya ngazi ya juu ya Umoja wa Mataifa

Miongoni utakayo sikia kwenye jarida hii leo ni pamojana Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassana ahutubia mkutano wa 76 wa Baraza Kuu la Umoja wa mataifa, UNGA76 akizungumziamasuala kadhaa ikiwemo ushirikiano wa kimataifa na ahadi yake kwa jumuiya ya kimataifa. Halikadhalika tunakwenda Ethiopia na pia Cameroon. Makala ni Uganda na mashinani tunakutana na Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya, karibu na mwenyeji wako ni Flora Nducha.

Sauti
9'56"
Wakulima wakilisha mifugo Ethiopia.
FAO/IFAD/WFP/Petterik Wiggers

Mradi wa IFAD umeongeza siyo tu milo bora bali pia kipato- Wakulima Ethiopia

Mkutano wa ngazi ya juu wa Umoja wa Mataifa umefanyika hii leo jiijni New York, Marekani kando mwa mjadala mkuu wa mkutano wa 76 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA76 ambapo vioingozi wa nchi 193 wa Umoja huo wamejadili mifumo endelevu ya chakula ya kuwezesha wakulima kulima mazao bila vikwazo na vile vile kuzalisha vyakula vyenye lishe sambamba na kuongeza kipato.
 

Sauti
1'39"