Mkutano wa 74 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa unaanza mwezi huu wa Septemba hadi wiki ya pili ya mwezi Septemba mwakani. Katika ukurasa huu hata hivyo tutakuwa tunakuletea habari motomoto kutoka mjadala wa wazi na vikao vya ngazi ya juu vya mkutano huo ambavyo vinafanyika kuanzia tarehe 22 septemba 2019 hadi 30 Septemba 2019. Pamoja na hotuba za viongozi ni vikao vya ngazi ya juu kuhusu Mkutano wa vijana wa vijana na mabadiliko ya tabianchi, fursa ya afya kwa wote, mkutano kuhusu fursa ya afya kwa wote, tathimini ya hatua za utekelezaji wa malengo ya maendeleo endelevu, ufadhili kwa ajili ya maendeleo na tathimini ya mwelekeo wa mkakati wa SAMOA.
MKUTANO WA 74 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA
Asilani hatutotiwa woga na vitisho:China
Katika hotuba yake kwenye mjadala Mkuu wa Baraza kuu la Umoja wa Mataifa siku ya Ijumaa Diwani wa jimbo na waziri wa mambo ya nje wa Uchina ametangaza kwamba nchi yake asilani haitotiwa woga na vitisho au kukubali shinikizo wakati inapokabiliwa na changamoto za ulinzi.
Tuwajibike wote kudhibiti kuenea kwa nyuklia- Urusi
Urusi imezungumzia mtazamo wake kuhusu hali inayoendelea nchini Iran, mzozo nchini Syria, vibali vya kuingia Marekani kwa maafisa wake wa kibalozi na masuala mengine nyeti kwenye ajenda ya kimataifa.
Tanzania tumedhamiria kubadili maisha ya watu wetu:Kabudi
Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki wa Tanzania Profesa Palamagamba John Kabudi amesema Tanzania imedhamiria kubadili maisha ya wananchi wake ikijitahidi kutekeleza malengo ya maendeleo endelevu SDGs.
Tufanye kazi na wanaoamini kwenye mabadiliko ya tabianchi- Kabudi
Mjadala Mkuu wa mkutano wa 74 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA74, ukiingia siku ya nne hii leo kwenye makao makuu ya umoja huo jijini New York, Marekani, Tanzania imesema imetenga asilimia 32 ya eneo la nchi kama hifadhi ya misitu kama njia mojawapo ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.
UN yatathimini hatua zilizopigwa mchakato wa SAMOA kuhusu visiwa vidogo vinavyoendelea
Wakuu wa nchi na viongozi wa serikali ni miongoni mwa waliokusanyika kwenye Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa leo Ijumaa Septemba 27 kushiriki mkutano maalum wa tathimini ya hatua zilizopigwa na nchi za visiwa vidogo zinazoendelea (SIDS) akiwemo Rais wa Ireland, Kenya na waziri mkuu wa Fiji na Norway.
Tanzania, Burundi na Kenya na ujumbe wao kwa Mkutano Mkuu wa Baraza Kuu la UN, UNGA74
Sasa ni mada kwa kina tukimulika kile ambacho Kenya, Burundi na Tanzia zimewasilisha mbele ya viongozi w anchi 193 wanachama wa Umoja wa Mataifa wakati wiki hii ya mjadala mkuu kwa lengo la kufanikisha ajenda ya maendeleo endelevu SDGs sambamba na amani, usalama na haki za binadamu.
Tusipoteze muda na wasioamini kwenye mabadiliko ya tabianchi- Tanzania
Mjadala Mkuu wa mkutano wa 74 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA74, ukiingia siku ya nne hii leo kwenye makao makuu ya umoja huo jijini New York, Marekani, Tanzania imesema imetenga asilimia 32 ya eneo la nchi kama hifadhi ya misitu kama njia mojawapo ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.