Mkutano wa 74 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa unaanza mwezi huu wa Septemba hadi wiki ya pili ya mwezi Septemba mwakani. Katika ukurasa huu hata hivyo tutakuwa tunakuletea habari motomoto kutoka mjadala wa wazi na vikao vya ngazi ya juu vya mkutano huo ambavyo vinafanyika kuanzia tarehe 22 septemba 2019 hadi 30 Septemba 2019. Pamoja na hotuba za viongozi ni vikao vya ngazi ya juu kuhusu Mkutano wa vijana wa vijana na mabadiliko ya tabianchi, fursa ya afya kwa wote, mkutano kuhusu fursa ya afya kwa wote, tathimini ya hatua za utekelezaji wa malengo ya maendeleo endelevu, ufadhili kwa ajili ya maendeleo na tathimini ya mwelekeo wa mkakati wa SAMOA.
MKUTANO WA 74 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA
Asanteni kwa kutambua dharura ya tabianchi ni vita vya maisha kwa ajili ya mutakabalki wetu-Guterres
Baada ya mjadala wa siku nzima wa mkutano maalum kwa ajili ya hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema amewashukuru vijana kote duniani kwa kuongoza mapambano na kukibebesha wajibu kizazi cha sasa.
Katibu Mkuu amuhakikishia rais wa DRC msaada wa kupambana na Ebola
Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, leo amekutana na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kandoni mwa mkutano wa ngazi ya Baraza Kuu la Umoja huo unaoendelea jijini New York Marekani.
Afya bora huwapa watu utu na matumaini na ndivyo tufanyavyo Rwanda:Kagame
Afya bora huwapa watu ut una kuwawezesha kufikia kilele cha mafanikio yao kwani ndio msingi wa maendeleo katika jamii.
Greta Thunberg ahoji uthubutu wa viongozi kusalia na maneno huku watu wakipoteza maisha
Leo katika ufunguzi wa mkutano wa ngazi ya juu wa viongozi wa Umoja wa Mataifa kuhusu hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Gutrerres amesema hatakuwa mtamazaji aliye kimya kwa uhalifu ambao unaathiri hali ya sasa na kuharibu haki kwa vizazi vijavyo kwa ajili ya mustakabali endelevu akiongeza kwamba viongozi wana haki ya kufanya kila wawezalo kukomesha janga la mabadiliko ya tabianchi kabla halijatukomesha.
Azimio la kisiasa lapitishwa kuchochea afya kwa wote ifikapo mwaka 2030
Viongozi wa dunia leo wamepitisha azimio la kisiasa lenye lengo la kuhakikisha afya kwa wote ifikapo mwaka 2030.
WHO yazisihi nchi ziwekeze asilimia 1 katika huduma za afya kwa wote
Nchi ni lazima ziongeze matumizi kwenye huduma za kimsingi za afya kwa takriban asiliamia 1 ya pato loa la kitaifa ikiwa dunia inataka kupunguza mianya ya kutimiza malengo ya afya ifikapo mwaka 2015, kwa mujibu wa ripoti mpya kutoka kwa Shirika la Afya Duniani na washirika kabla ya mkutano mkuu wa Umoja wa Mataifa kwa huduma za afya zilizo muhimu.
23 Septemba 2019
Miongoni mwa atakayokuletea Grace Kaneiya kwenye Jarida la Umoja wa Mataifa
-Bila kutimiza huduma za afya na za msingi kwa jamii zote duniani utekelezaji wa SDGs waninekana kama ndoto kwa mujibu wa WHO na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa
-Nchini Uganda wanaichi wanena kuhusu changamoto za huduma za afya
-Wakati wa kuchukua hatua dhidi ya tabia nchi ni sasa kunusuru kizazi kilichopo na kijacho wasema Umoja wa mataifa kwenye mkutano dhidi ya tabianchi
Lengo langu ni kuona vijana wanashiriki kilimo chenye tija na si bora kilimo - Mugo
Viongozi wa dunia wakikutana leo kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York Marekani kupitia azimio la kusongesha hatua kwa tabianchi, nchini Kenya vijana hivi sasa wanashiriki katika kilimo si tu chenye kuwawezesha kupata kipato bali pia kile kinacholinda na kuhifadhi mazingira lakini wanataka msaada zaidi ili waweze kusonga mbele.
Azimio la kisiasa lapitishwa kuchochea afya kwa wote ifikapo 2030
Viongozi wa dunia leo wamepitisha azimio la kisiasa lenye lengo la kuhakikisha afya kwa wote ifikapo mwaka 2030.
Nchi ziwekeze asilimia 1 katika huduma za afya kwa wote, WHO
Nchi ni lazima ziongeze matumizi kwenye huduma za kimsingi za afya kwa takriban asiliamia 1 ya pato loa la kitaifa ikiwa dunia inataka kupunguza mianya ya kutimiza malengo ya afya ifikapo mwaka 2015, kwa mujibu wa ripoti mpya kutoka kwa Shirika la Afya Duniani na washirika kabla ya mkutano mkuu wa Umoja wa Mataifa kwa huduma za afya zilizo muhimu.