Mkutano wa 74 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa unaanza mwezi huu wa Septemba hadi wiki ya pili ya mwezi Septemba mwakani. Katika ukurasa huu hata hivyo tutakuwa tunakuletea habari motomoto kutoka mjadala wa wazi na vikao vya ngazi ya juu vya mkutano huo ambavyo vinafanyika kuanzia tarehe 22 septemba 2019 hadi 30 Septemba 2019. Pamoja na hotuba za viongozi ni vikao vya ngazi ya juu kuhusu Mkutano wa vijana wa vijana na mabadiliko ya tabianchi, fursa ya afya kwa wote, mkutano kuhusu fursa ya afya kwa wote, tathimini ya hatua za utekelezaji wa malengo ya maendeleo endelevu, ufadhili kwa ajili ya maendeleo na tathimini ya mwelekeo wa mkakati wa SAMOA.
MKUTANO WA 74 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA
Je wajua mapana na marefu ya rungu la kuongozea mikutano ya UNGA?
Rungu la rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA, linalotumiwa kuongozea mikutano lilitolewa kama zawadi ya Iceland kwa Umoja wa Mataifa.
Vijana tunahitaji uhuru wa kutoa mawazo kuleta mabadiliko chanya- Wanjuhi
Ikiwa kesho jumamosi vijana kutoka nchi mbalimbali wanachama wa Umoja wa Mataifa wanakutana jijini New York, Marekani katika jukwaa lao, Wanjuhi Njoroge, mwanaharakati kutoka Kenya ambaye atahutubia jukwaa hilo kubwa zaidi kuwahi kuandaliwa na Umoja wa Mataifa amesema kile ambacho atapaza katika ujumbe wake.
Matarajio ya wiki ya mjadala mkuu wa Baraza Kuu na Balozi Mero
Katika kuelekea wiki ya vikao vya mjadala mkuu wa Baraza Kuu vitakavyowakutanisha viongozi wa dunia katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York Marekani, tunaye Mwakilishi wa kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Modest Mero kuchambua yatakayojiri.
Vijana katika nchi chafuzi wa mazingira tambueni madhara upande mmoja hutugusa sote- Wanjuhi
Ikiwa kesho jumamosi vijana kutoka nchi mbalimbali wanachama wa Umoja wa Mataifa wanakutana jijini New York, Marekani katika jukwaa lao, Wanjuhi Njoroge, mwanaharakati kutoka Kenya ambaye atahutubia jukwaa hilo kubwa zaidi kuwahi kuandaliwa na Umoja wa Mataifa amesema kile ambacho atapaza katika ujumbe wake.
Kutowashirikisha vijana kwenye tabianchi ni janga- Guterres
Kuelekea siku ya kimataifa ya amani ambayo huadhimishwa kila mwaka Septemba 21, leo katika maadhimisho kwenye Umoja wa Mataifa Katibu Mkuu wa Umoja huo, Antonio Guterres ametoa wito wa hatua madhubuti kuchukuliwa kukabiliana na changamoto kubwa za dunia ikiwemo mabadiliko ya tabianchi ili kudumisha amani kwa wote.