Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

MKUTANO WA 74 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA

MKUTANO WA 74 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA
MJADALA MKUU WA UNGA74

Mkutano wa 74 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa unaanza mwezi huu wa Septemba hadi wiki ya pili ya mwezi Septemba mwakani. Katika ukurasa huu hata hivyo tutakuwa tunakuletea habari motomoto kutoka mjadala wa wazi na vikao vya ngazi ya juu vya mkutano huo ambavyo vinafanyika kuanzia tarehe 22 septemba 2019 hadi 30 Septemba 2019. Pamoja na hotuba za viongozi ni vikao vya ngazi ya juu kuhusu  Mkutano wa vijana wa vijana na mabadiliko ya tabianchi, fursa ya afya kwa wote, mkutano kuhusu fursa ya afya kwa wote, tathimini ya hatua za utekelezaji wa malengo ya maendeleo endelevu, ufadhili kwa ajili ya maendeleo na tathimini ya mwelekeo wa mkakati wa SAMOA.

Wanjuhi Njoroge, mwanaharkati kijana wa mazingira kutoka Kenya na mshiriki wa kongamano la vijana kuhusu hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi.
UNnewskiswahili/Patrick Newman

Vijana katika nchi chafuzi wa mazingira tambueni madhara upande mmoja hutugusa sote- Wanjuhi

Ikiwa kesho jumamosi vijana kutoka nchi mbalimbali wanachama wa Umoja wa Mataifa wanakutana jijini New York, Marekani katika jukwaa lao, Wanjuhi Njoroge, mwanaharakati kutoka Kenya ambaye atahutubia jukwaa hilo kubwa zaidi kuwahi kuandaliwa na Umoja wa Mataifa amesema kile ambacho atapaza katika ujumbe wake.

Sauti
2'15"
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa akiwa katika mahojiano maalumu na Mkuu wa Idara ya mawasiliano ya umma ya Umoja wa Mataifa Melissa Fleming mjini New York Marekani Septemba 18, 2019.
UN News/Ben Lybrand

Kutowashirikisha vijana kwenye tabianchi ni janga- Guterres

Kuelekea siku ya kimataifa ya amani ambayo huadhimishwa kila mwaka Septemba 21, leo katika maadhimisho kwenye Umoja wa Mataifa Katibu Mkuu wa Umoja huo, Antonio Guterres ametoa wito wa hatua madhubuti kuchukuliwa kukabiliana na changamoto kubwa za dunia ikiwemo mabadiliko ya tabianchi ili kudumisha amani kwa wote. 

Sauti
3'12"