Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

MKUTANO WA 74 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA

MKUTANO WA 74 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA
MJADALA MKUU WA UNGA74

Mkutano wa 74 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa unaanza mwezi huu wa Septemba hadi wiki ya pili ya mwezi Septemba mwakani. Katika ukurasa huu hata hivyo tutakuwa tunakuletea habari motomoto kutoka mjadala wa wazi na vikao vya ngazi ya juu vya mkutano huo ambavyo vinafanyika kuanzia tarehe 22 septemba 2019 hadi 30 Septemba 2019. Pamoja na hotuba za viongozi ni vikao vya ngazi ya juu kuhusu  Mkutano wa vijana wa vijana na mabadiliko ya tabianchi, fursa ya afya kwa wote, mkutano kuhusu fursa ya afya kwa wote, tathimini ya hatua za utekelezaji wa malengo ya maendeleo endelevu, ufadhili kwa ajili ya maendeleo na tathimini ya mwelekeo wa mkakati wa SAMOA.

UN /Kim Haughton

Tusijisahau, wakazi wa dunia wana matarajio makubwa na UN-Balozi Bande

Hatimaye kikao cha kwanza cha mkutano wa 74 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kimeanza leo kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani chini ya uongozi wa Rais wake Balozi Tijjani Muhammad-Bande kutoka Nigeria.

Kikao kilianza kwa Balozi Bande kugonga nyundo hiyo ya kuitisha wajumbe ili waketi tayari kwa shughuli za siku hiyo.

Kisha akatangazia wajumbe wasimame kwa dakika moja, ikiwa ni tamaduni ya kuanza kwa kikao kwa maombi na tafakuri.

Sauti
3'20"
Kituo cha kawi kutokana na nishati ya jua.
World Bank/Dana Smillie

Mabadiliko ya tabianchi

Umoja wa Mataifa unajitayarisha kwa ajili mkutano wa “Kuchukua Hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi Septemba mwaka wa 2019 huko New York, Marekani ambao ni moja ya mikutano ya ngazi ya juu ya tabianchi katika siku za karibuni, cha kujiuliza nihatua gani ambayo ulimwengu umepiga katika kukabiliana na shida ya tabianchi, na maendeleo hayo yanapimwaje?