Mkutano wa 74 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa unaanza mwezi huu wa Septemba hadi wiki ya pili ya mwezi Septemba mwakani. Katika ukurasa huu hata hivyo tutakuwa tunakuletea habari motomoto kutoka mjadala wa wazi na vikao vya ngazi ya juu vya mkutano huo ambavyo vinafanyika kuanzia tarehe 22 septemba 2019 hadi 30 Septemba 2019. Pamoja na hotuba za viongozi ni vikao vya ngazi ya juu kuhusu Mkutano wa vijana wa vijana na mabadiliko ya tabianchi, fursa ya afya kwa wote, mkutano kuhusu fursa ya afya kwa wote, tathimini ya hatua za utekelezaji wa malengo ya maendeleo endelevu, ufadhili kwa ajili ya maendeleo na tathimini ya mwelekeo wa mkakati wa SAMOA.
MKUTANO WA 74 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA
Tusijisahau, wakazi wa dunia wana matarajio makubwa na UN-Balozi Bande
Hatimaye kikao cha kwanza cha mkutano wa 74 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kimeanza leo kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani chini ya uongozi wa Rais wake Balozi Tijjani Muhammad-Bande kutoka Nigeria.
Kikao kilianza kwa Balozi Bande kugonga nyundo hiyo ya kuitisha wajumbe ili waketi tayari kwa shughuli za siku hiyo.
Kisha akatangazia wajumbe wasimame kwa dakika moja, ikiwa ni tamaduni ya kuanza kwa kikao kwa maombi na tafakuri.
Jamani tusisahau kuwa dunia ina matarajio makubwa na UN- Balozi Bande
Hatimaye kikao cha kwanza cha mkutano wa 74 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kimeanza leo kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani chini ya uongozi wa Rais wake Balozi Tijjani Muhammad-Bande kutoka Nigeria.
Mabadiliko ya tabianchi
Umoja wa Mataifa unajitayarisha kwa ajili mkutano wa “Kuchukua Hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi Septemba mwaka wa 2019 huko New York, Marekani ambao ni moja ya mikutano ya ngazi ya juu ya tabianchi katika siku za karibuni, cha kujiuliza nihatua gani ambayo ulimwengu umepiga katika kukabiliana na shida ya tabianchi, na maendeleo hayo yanapimwaje?
Rais mteule wa UNGA74 ataja vipaumbele vyake
Rais mteule wa Baraza Kuu la Umoja wa Umoja wa Mataifa Balozi Tijjani Muhammad-Bande ametaja vipaumbele vyake vitatu kuwa ni umaskini, elimu bora na ujumuishaji wa kila mtu.
Umaskini, elimu na ujumuishaji ni vipaumbele vya kwanza katika orodha ya vipaumbele vya Rais mpya wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa
Mkutano wa 74 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, ukianza rasmi leo kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani, Rais mteule wa mkutano huo Balozi Tijjani Muhammad-Bande ametaja vipaumbele vyake vitatu kuwa ni umaskini, elimu bora na ujumuishaji wa kila mtu.