Mkutano wa 73 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa unaanza mwezi huu wa Septemba hadi wiki ya pili ya mwezi Septemba mwakani. Katika ukurasa huu hata hivyo tutakuwa tunakuletea habari motomoto kutoka mjadala wa wazi na vikao vya ngazi ya juu vya mkutano huo ambavyo vinafanyika kuanzia tarehe 25 septemba 2018 hadi Oktoba mosi 2018. Pamoja na hotuba za viongozi ni vikao vya ngazi ya juu kuhusu Kifua Kikuu, Ulinzi wa Amani, tukio maalum la kumuenzi hayati Nelson Mandela na magonjwa yasiyo ya kuambukiza, NCDs.
MKUTANO WA 73 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA
Darfur ya sasa ni bora kuliko miaka 10 nyuma, lakini kazi bado ipo – Naibu Katibu Mkuu UN
Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Bi. Amina Mohammed amesema hivi sasa jimbo la Darfur ya sasa nchini Sudan inaonekaana ni tofauti na Darfur ya miaka 10 iliyopita wakati ambapo Muungano wa Afrika, AU wa Afrika na Umoja wa Mataifa kwa pamoja walituma vikosi vya kulinda amani.
Sudan Kusini tunapiga hatua,asanteni sana- Gai
Mwaka jana nilisimama mbele yenu nikiwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa nchi iliyogubikwa na vita. Leo hii nimesimama tena mbele yenu kama shuhuda wa kile ambacho wanachama wa chombo hiki adhimu wamesaidia kufanikisha ndani ya Jamhuri ya Sudan Kusini.
Ni kauli ya Taban Deng Gai, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Sudan Kusini aliyotoa wakati akihutubia mjadala mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa unaoendelea kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York, Marekani.
Sudan Kusini ya mwaka jana si ya mwaka huu, shukrani UN, AU na wadau- Gai
Mwaka jana nilisimama mbele yenu nikiwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa nchi iliyogubikwa na vita. Leo hii nimesimama tena mbele yenu kama shuhuda wa kile ambacho wanachama wa chombo hiki adhimu wamesaidia kufanikisha ndani ya Jamhuri ya Sudan Kusini.
Uhamiaji sio shida Afrika la msingi kutovunja sheria- Rais Nyusi
Suala la uhamiaji likiendelea kuibua vuta nikuvute, Msumbiji imesema kuwa la msingi ni watu kufuata sheria kwani uhamiaji umekuwepo na utaendelea kuwepo.