Mkutano wa 73 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa unaanza mwezi huu wa Septemba hadi wiki ya pili ya mwezi Septemba mwakani. Katika ukurasa huu hata hivyo tutakuwa tunakuletea habari motomoto kutoka mjadala wa wazi na vikao vya ngazi ya juu vya mkutano huo ambavyo vinafanyika kuanzia tarehe 25 septemba 2018 hadi Oktoba mosi 2018. Pamoja na hotuba za viongozi ni vikao vya ngazi ya juu kuhusu Kifua Kikuu, Ulinzi wa Amani, tukio maalum la kumuenzi hayati Nelson Mandela na magonjwa yasiyo ya kuambukiza, NCDs.
MKUTANO WA 73 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA
Uganda itaendelea kuwa kimbilio la wakimbizi- Rugunda
Sisi ni kizazi cha kutokomeza njaaTunaweza kuwa kizazi cha kwanza kufanikiwa kutokomeza njaa, kama ambavyo tunaweza kuwa kizazi cha mwisho kuikoa dunia.
Tunaunga mkono ushirikiano wa kimataifa- Tanzania
Tanzania imetaka hatua za dhati zichukuliwe ili kuokoa hoja ya ushirikiano wa kimataifa ambao hivi sasa uko mashakani.
Hongera Sudan Kusini kwa kuchukua hatua zaidi kuwalinda watoto:Gamba
Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwa ajili ya watoto na migogoro ya Silaha, Bi. Virginia Gamba, ameipongeza serikali ya Sudan Kusini kwa kuongeza kipengele cha hiyari kwenye mkataba kuhusu haki za mtoto katika ushirikishaji kwenye migogoto ya kivita (OPAC).
Israel yadai imebaini bohari la siri la silaha za atomiki nchini Iran
Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amehutubia mjadala mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mjini New York, Marekani huku akijinasibu kuwa wamebaini bohari la kisiri la silaha za atomiki nchini Iran lenye tani 300 za vifaa vya nyuklia.
Tungearifiwa tungeshiriki mkutano leo kuhusu Afrika ya Kati:DRC
Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, imesema imeamua kutoshiriki mkutano maalumu wa ngazi ya juu wa mawaziri ulioandaliwa kandoni mwa mjadala wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kuhusu masuala yanayolighubika eneo la Afrika ya Kati ikiwemo DRC.
"Amani na usalama wa dunia uko mikononi mwetu viongozi"- Rais Masisi wa Botswana
Rais wa Botswana Mokgweetsi Masisi akihutubia mjadala mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa hii leo mjini New York, Marekani, amezitaka pande zote zilizoko katika migogoro kote duniani kufikiria juu ya wananchi wao na kuhakikisha zinawajibika kuwalinda kwa mujibu wa haki na sheria za kimataifa za haki za binadamu.
Hakuna mwanamke anayestahili kuuawa kwasababu ya jinsia yake:UN-EU
Umoja wa Mataifa na Muungano wa Ulaya EU leo wamezindua mkakati wa kukomesha mauaji dhidi ya wanawake na wasicha katika nchi tano za Amerika ya Kuisni kwa sababu tu ya jinsia yao, mkakati ujulikanao kama Spotlight.
Dkt. Tedros aonyesha picha halisi ya NCDs duniani, wajumbe waonyesha simanzi
Simanzi ilionekana leo kwenye nyuso za washirki wa mkutano wa ngazi ya juu kuhusu magonjwa yasiyo ya kuambukiza baada ya Mkurugenzi Mkuu wa shirika la afya duniani, WHO, Dkt. Tedros Ghebreyesus kuomba washiriki wasimame pindi tu wanaposikia ametaja ugonjwa ambao umekuwa chanzo cha kifo cha iwe ndugu, jamaa, jirani au rafiki.
Tanzania kutangaza msimamo wake kwa UN
Tanzania itatumia mjadala mkuu wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, kutangaza msimamo wake na chombo hicho chenye wanachama 193. Taarifa zaidi na Assumpta Massoi.