Mkutano wa 73 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa unaanza mwezi huu wa Septemba hadi wiki ya pili ya mwezi Septemba mwakani. Katika ukurasa huu hata hivyo tutakuwa tunakuletea habari motomoto kutoka mjadala wa wazi na vikao vya ngazi ya juu vya mkutano huo ambavyo vinafanyika kuanzia tarehe 25 septemba 2018 hadi Oktoba mosi 2018. Pamoja na hotuba za viongozi ni vikao vya ngazi ya juu kuhusu Kifua Kikuu, Ulinzi wa Amani, tukio maalum la kumuenzi hayati Nelson Mandela na magonjwa yasiyo ya kuambukiza, NCDs.
MKUTANO WA 73 WA BARAZA KUU LA UMOJA WA MATAIFA
Madiba hakupenda makuu
Ikiwa leo Umoja wa Mataifa unafanya tukio maalum kuhusu miaka 100 tangu kuzaliwa rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini, hayati Nelson Mandela, mwanadiplomasia nguli nchini Tanzania na ambaye amewahi kuhudumu barani Afrika na Umoja wa Mataifa amemmwagia sifa hayati Mandela akisema kuwa alikuwa kiongozi shupavu ambaye kisasi chake baada ya kufungwa kilikuwa ni kuona watu wake wanaendelea.
Viongozi wa sasa waige mfano wa Mandela- Dkt. Salim
Mwendazake Mzee Nelson Mandela, angalikuwa anatimiza umri wa miaka 100 mwaka huu iwapo angalikuwa hai. Ingawa hayupo, bado kile alichokifanya wakati wa uhai wake kinakumbukwa na kuenziwa siyo tu nchini mwake na barani Afrika bali pia katika Umoja wa Mataifa ambako ajenda alizokuwa anatetea ni mambo ambayo ni msingi wa Umoja wa Mataifa.
Matarajio yetu kwa dunia iliyo sawa ni kwenu vijana: Guterres
Umoja wa Mataifa leo umezindua mkakati wake mpya wa kuimarisha mchango wa takribani vijana bilioni 2 duniani kwa lengo kukuza amani, uadilifu pamoja na kuwa na dunia endelevu.
Uhamiaji Afrika si karaha bali ni faida:UNCTAD
Kuuchukulia uhamiaji kama ni tatizo si fikra nzuri , kwani unahamiaji una faida nyingi, kwa wahamiaji wenyewe lakini pia kwa jamii zinazowahifadhi, iwe katika masuala ya kiuchumi, utamaduni na hata maendeleo kwa mujibu wa Kamati ya Umoja wa Mataifa ya biashara na maendeleo UNCTAD
Tutumie busara za Mandela kukabili changamoto za sasa- Guterres
Umoja wa Mataifa leo umepitisha azimio la kumuenzi Nelson Mandela kutokana na mchango wake katika kusongesha utu, amani na haki za binadamu siyo tu nchini mwake bali duniani kote kwa ujumla. Taarifa zaidi na Grace Kaneiya.
Kwanini Brazil huwa ya kwanza kuhutubia UNGA?
Kawaida ni rais wa Brazil ndiye hufungua vikao vya ngazi za juu katika Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa. Lakini ni kwa nini? Utaratibu huu ulianza katika kikao cha mwanzo kabisa kilichofanyika mjini London, Uingereza Januari 10 mwaka 1946. Tangu wakati huo Brazil imekuwa kila mara inakuwa ya kwanza katika ratiba za viongozi kuhutubia mjadala wa wazi wa Baraza hilo unaofanyika kila mwezi Septemba.
Kisasi cha Mandela baada ya kutoka gerezani ni cha kuigwa- Dkt. Salim
Mwanadiplomasia nguli ambaye amewahi kufanya kazi na hayati Mzee Nelson Mandela azungumzia upekee aliokuwa nao mwendazake huyo ambaye leo anaenziwa na UN
Mandela kuenziwa leo kwenye UN; Azimio maalum kupitishwa
Leo katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York Marekani, nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa wanapitisha azimio la kumuenzi aliyekuwa Rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini, Hayati Nelson Mandela.
Hayati Mandela angalikuwa hai mwaka huu, angalikuwa anatimiza umri wa miaka 100 tangu kuzaliwa kwake.
Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa imezungumza na Mwakilishi wa kudumu wa Tanzania kwenye Umoja wa Mataifa Balozi Modest Mero na kumuuliza kiini hasa cha nchi wanachama kuamua kupitisha azimio hilo kuhusu Mandela ambapo amesema.
Dunia ijifunze kusamehe kama alivyofanya Mandela- Balozi Mero
Leo katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York Marekani, nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa wanapitisha azimio la kumuenzi aliyekuwa Rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini, Hayati Nelson Mandela.