Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UDHR70

UDHR70
Tamko la Haki za Binadamu la UN-Uchambuzi wa Ibara

Tamko la haki za binadamu la Umoja wa Mataifa, UDHR, ni nyaraka ya kihistoria iliyopitishwa na nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa mwaka 1948 kwa lengo la kuhakikisha haki za binadamu zinalindwa. Rasimu ya nyaraka hii iliandaliwa na wawakilishi wenye usuli tofauti kuanzia sheria hadi utamaduni na walitoka maeneo yote ya dunia. Baada ya kuiandaa na kuijadili rasimu hiyo ilipitishwa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa tarehe 10 Disemba mwaka 1948 mjini Paris, Ufaransa kwa azimio namba 217 A la baraza hilo. Likipatiwa jina la tamko la haki za binadmu, nyaraka hiyo inaweka viwango vya pamoja vya haki za binadamu kwa wote na mataifa yote. Azimio hilo, kwa mara ya kwanza liliweka misingi ya haki za binadamu inayokubalika kimataifa na inayopaswa kulindwa popote pale duniani. Hadi sasa nyaraka hiyo imetafsiriwa kwa zaidi ya lugha 500 ikiwemo Kiswahili.

Pata taarifa kila wakati pindi tunapochapisha taarifa mpya kwa kujisajili

Utekelezaji wa ibara 13 Kenya ni mzuri licha ya changamoto

Ibara ya 13 ya tamko la haki za binadamula Umoja wa Mataifa ambalo linatimiza miaka sabini mwaka huu inasema, kila mtu ana haki ya uhuru wa kutembea na kuishi ndani ya mipaka ya nchi yake - Na kila mtu ana haki ya kuondoka na kurudi nchini mwake. 

Nchini Kenya haki hii ipo kwenye katiba ambapo Robi Chacha, Afisa kampeni usalama na haki za bindamu katika shirika lisilo la kiserikali la Amnesty International, nchini humo anasema utekelezaji wake unaridhisha.

Sauti
3'37"

Nchi zinatakiwa kubadili sheria zao ili kwenda sawa na mbinu za sasa za utumwa na utwana.

Ibara ya 4 ya tamko la haki za binadamu la Umoja wa Mataifa linalotimiza miaka 70 mwaka huu wa 2018, inaeleza kinagaubaga kuwa hakuna mtu anayestahili kugeuzwa mtumwa na wala kuwa mtwana wa mtu yeyote. Na ingawa kwa miaka mingi nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa zimeridhia na pia kutunga sheria za kuunga mkono ibara hii, mabadiliko ya namna utumwa na utwana unavyotafsiriwa yaneziacha nyuma sheria nyingi. Wakili Jebra Kambole wa Tanzania katika mazungumzo haya na Arnold Kayanda, anasema kuna haja ya jumuiya ya kimataifa kulitizamasuala hili kwa namna mpya.

Sauti
2'51"

Ibara kwa Ibara- Tamko la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa

Kila mtu anastahili kuwa na haki zote na uhuru wote ambao umeelezwa katika tamko hili bila ubaguzi wa aina yoyote kama vile rangi, taifa, jinsia, lugha, dini, siasa, fikra, asili ya taifa la mtu, miliki , kuzailiwa au kwa hali nyingine yoyote.

Halikadhalika hakuna ubaguzi utakaotendwa kwa misingi ya kisiasa, kimamlaka au hadhi ya kimataifa ya nchi au utawala ambao mtu fulani anatoka, iwe ni huru, iwe chini ya  udhamini, isiyojitawala au chini ya mazingira mengine yenye udhibiti wa kimamlaka.

Sauti
52"