Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UDHR70

UDHR70
Tamko la Haki za Binadamu la UN-Uchambuzi wa Ibara

Tamko la haki za binadamu la Umoja wa Mataifa, UDHR, ni nyaraka ya kihistoria iliyopitishwa na nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa mwaka 1948 kwa lengo la kuhakikisha haki za binadamu zinalindwa. Rasimu ya nyaraka hii iliandaliwa na wawakilishi wenye usuli tofauti kuanzia sheria hadi utamaduni na walitoka maeneo yote ya dunia. Baada ya kuiandaa na kuijadili rasimu hiyo ilipitishwa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa tarehe 10 Disemba mwaka 1948 mjini Paris, Ufaransa kwa azimio namba 217 A la baraza hilo. Likipatiwa jina la tamko la haki za binadmu, nyaraka hiyo inaweka viwango vya pamoja vya haki za binadamu kwa wote na mataifa yote. Azimio hilo, kwa mara ya kwanza liliweka misingi ya haki za binadamu inayokubalika kimataifa na inayopaswa kulindwa popote pale duniani. Hadi sasa nyaraka hiyo imetafsiriwa kwa zaidi ya lugha 500 ikiwemo Kiswahili.

Pata taarifa kila wakati pindi tunapochapisha taarifa mpya kwa kujisajili

Photo UNAMA / Abbas Naderi

Kubadili mifumo ndio muarobaini wa haki za huduma za jamii Tanzania: Dkt.Bisimba

Nchini Tanzania ingawa katika katiba  imeaainishwa haki za huduma za jamii kwa wote, mifumo iliyopo inafanya kuwa changamoto kubwa ya utekelezaji wa haki hizo. Hayo yamesemwa na Dkt.Helen Kijo Bisimba mwanaharakati wa muda mrefu wa haki za binadamu nchini humo. Akijadili ibara ya 21 ya tamko la haki za binadamu  isemayo “kila mtu ana haki ya kushiriki katika serikali yake, haki sawa za huduma za jamii ikiwa ni pamoja na serikali kuongoza kwa matakwa ya wananchi”, Dkt.

Sauti
5'29"

29 Novemba 2018

Leo katika Jarida la Habari la Umoja wa Mataifa Arnold Kayanda anakuletea

-Hatari ya VVU kwa vijana barubaru ifikapo 2030, barubaru 80 watapoteza maisha kila siku kama mwenendo hautobadilika limeonya shirika la UNICEF

-Umuhimu wa ushirika wa Kusini-Kusini kwa bara la Afrika ni mkubwa

-UNMISS kuongeza vikosi jimbo la Nile Sudan Kusini kwa ajili ya ulinzi wa raia

-Makala inamulika Ibara ya 21 ya tamko la haki za binadamu kuhusu "haki ya wananchi kushiriki katika serikali , huduma za jamii na uongozi kuzingatia matakwa ya wananchi".

Sauti
14'4"