Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UDHR70

UDHR70
Tamko la Haki za Binadamu la UN-Uchambuzi wa Ibara

Tamko la haki za binadamu la Umoja wa Mataifa, UDHR, ni nyaraka ya kihistoria iliyopitishwa na nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa mwaka 1948 kwa lengo la kuhakikisha haki za binadamu zinalindwa. Rasimu ya nyaraka hii iliandaliwa na wawakilishi wenye usuli tofauti kuanzia sheria hadi utamaduni na walitoka maeneo yote ya dunia. Baada ya kuiandaa na kuijadili rasimu hiyo ilipitishwa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa tarehe 10 Disemba mwaka 1948 mjini Paris, Ufaransa kwa azimio namba 217 A la baraza hilo. Likipatiwa jina la tamko la haki za binadmu, nyaraka hiyo inaweka viwango vya pamoja vya haki za binadamu kwa wote na mataifa yote. Azimio hilo, kwa mara ya kwanza liliweka misingi ya haki za binadamu inayokubalika kimataifa na inayopaswa kulindwa popote pale duniani. Hadi sasa nyaraka hiyo imetafsiriwa kwa zaidi ya lugha 500 ikiwemo Kiswahili.

Pata taarifa kila wakati pindi tunapochapisha taarifa mpya kwa kujisajili

Jinamizi la kutosajiliwa utotoni, laandama maelfu ya watu wasio na utaifa

Ibara ya 15 ya tamko la haki za binadamu la Umoja wa Mataifa linasisitiza haki ya mtu kuwa na utaifa. Iwe ni utaifa kwa kuzaliwa au kwa kusajiliwa katika nchi nyingine. Hata hivyo kutokana na sababu mbalimbali zaidi ya watu milioni 12 hivi sasa duniani  hawana utaifa. Ukosefu wa utaifa  unapoka watoto na watu wazima haki zao za msingi. Je ni sababu gani basi zinafanya watu wakose utaifa, na ni madhila yapi basi wanapitia? Ungana basi na Grace Kaneiya katika makala hii.

Sauti
3'11"