Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
WHO yaeleza hofu yake kubwa zaidi juu ya virusi vya Corona
Shirika la afya ulimwenguni, WHO limesema kuwa hofu yake kubwa zaidi hivi sasa ni ugonjwa unaosababishwa na virusi vya Corona, COVID-19 kuingia katika mataifa yenye mifumo dhaifu ya afya hususan barani Afrika.
COVID-19 yaweza kuwa na madhara ya kiuchumi hata nje ya China- IMF
Wakati idadi ya maambukizi ya virusi vya corona COVID-19 ikiendelea kuongezeka kila uchao, Shirika la afya ulimwenguni, WHO limehimiza jamii ya kimataifa kuwekeza katika suluhu za afya ambazo zinaweza kusaidia katika kudhibiti mlipuko wa ugonjwa huo sasa na wakati huo huo kusaidia katika kujiandaa kwa ajili ya kuwekeza katika jamii kwa siku za usoni. Grace Kaneiya na ripoti kamili.
Wito huo umetolewa siku chache baada ya taarifa za shirika la fedha duniani, IMF ya makadirio yake kuhusu athari za mlipuko wa virusi vya corona kiuchumi.
WHO yaingiwa hofu na mwenendo wa maambukizi ya virusi vya Corona, COVID-19
Shirika la afya ulimwenguni, WHO, limesema hofya yake hivi sasa juu ya kuenea kwa virusi vya Corona, COVID-19 ni kutokuwa na taarifa za wazi kuhusu uhusiano wa kuenea kwa virusi hivyo, kama vile historia ya mtu kusafiri China au kuwa na mawasiliano na mtu aliyethibitishwa kuambukizwa virusi hivyo.
Athari za kiuchumi za virusi vya corona huenda zikasikika hadi nje ya China-IMF
Wakati idadi ya maambukizi ya virusi vya corona COVID-19 ikiendelea kuongezeka kila uchao, Shirika la afya ulimwenguni, WHO limehimiza jamii ya kimataifa kuwekeza katika suluhu za afya ambazo zinaweza kusaidia katika kudhibiti mlipuko wa ugonjwa huo sasa na wakati huo huo kusaidia katika kujiandaa kwa ajili ya kuwekeza katika jamii kwa siku za usoni.
Virusi vya COVID-19 sio hatari kama vilivyo virusi vingine vya aina hiyo-WHO
Shirika la afya ulimwenguni, WHO limesema inaonekana kwamba virusi vya corona COVID-19 sio hatari kama vilivyo virusi vingine vya aina hiyo ikiwemo vile vinavyosababisha homa ya mafua, SARS au virusi vya corona vinavyosababisha matatizo ya kupumua MERS na kuongeza kwamba asilimia 80 ya wagonjwa wana viwango vya chini vya virusi na watapona.
Vifo vya corona vyazidi 1000, WHO yaitisha jukwaa la utafiti na ubunifu
Shirika la afya duniani WHO linaendesha jukwaa la utafiti na ubunifu ili kuchukua hatua za kimataifa kushughulikia ,mlipuko wa virusi vya corona yaani COVID-2019 ambapo hadi sasa watu 42,000 wameambukizwa na tayari vifo vimefikia zaidi ya 1000.
WHO imehimiza umuhimu wa serikali kudhibiti virusi vya corona.
Shirika la afya ulimwenguni, WHO leo Jumatatu limehimiza umuhimu wa serikali kuendelea kuweka kipaumblele katika kuzuia na kudhibiti virusi vya corona.
Dunia inapungukiwa vifaa vya kujikinga wakati idadi ya waathirika wa corona ikipanda-WHO
Mkurugenzi Mkuu wa shirika la afya ulimwenguni WHO, Dkt Tedros Adhanom Ghebreyesus ameonya kuwa ulimwengu unakabiliwa na sintofahamu kubwa katika soko la vifaa vya kujikinga na kutoa wito kwa nchi na makampuni kufanya kazi na WHO "kuhakikisha matumizi sawa ya vifaa na kuzingatia mizania katika soko" katika kukabiliana na virusi vipya vya corona (2019-nCoV).
WHO kuimarisha utafiti na uvumbuzi kwa ajili ya kukabiliana nan virusi vya corona
Shirika la afya ulimwenguni, WHO imeandaa kongamano wa kimataifa wa utafiti na uvumbuzi kuchagiza hatua za kimataifa kukabiliana na virusi vipya vya corona.
Pamoja na mlipuko wa virusi vya corona China, waathirika wa VVU wataendelea kuangaliwa vizuri-UNAIDS
Shirika la Umoja wa Mataifa linalopambana na Virusi Vya UKIMWI na UKIMWI, UNAIDS limesema linafanya kazi kwa ukaribu kwa kushirikiana na mamalaka nchini China kuhakikisha pamoja na uwepo wa virusi vya corona, huduma kwa wagonjwa wa Virusi Vya ukimwi, VVU wanaendelea kupata huduma.